Zaburi 28:1-9
-
Sala ya mtunga zaburi yasikiwa
-
‘Yehova ni nguvu zangu na ngao yangu’ (7)
-
Wa Daudi.
28 Ninaendelea kukulilia wewe, Ee Yehova Mwamba wangu;+Usiwe kama kiziwi kwangu.
Ukininyamazia,Nitakuwa kama wale wanaoshuka shimoni.*+
2 Sikia sihi zangu ninapokulilia unisaidieNinapoinua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha mahali pako patakatifu.+
3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wanaotenda mambo yanayodhuru,+Wale wanaoongea na jirani yao maneno ya amani lakini uovu uko mioyoni mwao.+
4 Walipe kulingana na matendo yao,+Kulingana na mazoea yao maovu.
Walipe kulingana na kazi ya mikono yao,Kulingana na mambo waliyotenda.+
5 Kwa maana hawazingatii utendaji wa Yehova,+Wala kazi ya mikono yake.+
Atawabomoa kabisa naye hatawajenga.
6 Yehova na asifiwe,Kwa maana amesikia sihi zangu za kuomba msaada.
7 Yehova ni nguvu zangu+ na ngao yangu;+Moyo wangu unamtumaini yeye.+
Amenisaidia, na moyo wangu unashangilia,Kwa hiyo nitamsifu kwa wimbo wangu.
8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;Yeye ni ngome, anamletea mtiwa-mafuta wake wokovu mkubwa.+
9 Waokoe watu wako, na uubariki urithi wako.+
Wachunge na kuwabeba mikononi mwako milele.+
Maelezo ya Chini
^ Au “kaburini.”