Zaburi 141:1-10
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, ninakulilia wewe.+
Njoo haraka unisaidie.+
Sikiliza ninapokulilia.+
2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+Mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama toleo la jioni la nafaka.+
3 Weka mlinzi wa kinywa changu, Ee Yehova,Weka ulinzi kwenye mlango wa midomo yangu.+
4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote ovu,+Nisishirikiane na watu waovu kutenda mambo mapotovu;Nisile kamwe vyakula vyao vitamu.
5 Mwadilifu akinipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mshikamanifu;+Akinikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+Ambayo kichwa changu hakiwezi kamwe kukataa.+
Nitaendelea kusali hata wanapopatwa na misiba.
6 Ingawa waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye jabali,Watu watayasikiliza maneno yangu, kwa maana yanapendeza.
7 Kama mtu anavyolima na kuuvunja-vunja udongo,Ndivyo mifupa yetu ilivyotawanywa kwenye mlango wa Kaburi.*
8 Lakini macho yangu yanakutazama wewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+
Nimekukimbilia wewe.
Usiniue.*
9 Nilinde dhidi ya mataya ya mtego walionitegea,Dhidi ya mitego ya watenda maovu.
10 Waovu wote wataanguka pamoja ndani ya nyavu zao wenyewe+Huku nikipitia karibu nazo kwa usalama.