Zaburi 141:1-10

  • Sala ya kuomba ulinzi

    • ‘Sala yangu na iwe kama uvumba’ (2)

    • Karipio la mwadilifu ni kama mafuta (5)

    • Waovu wanaanguka ndani ya nyavu zao wenyewe (10)

Muziki wa Daudi. 141  Ee Yehova, ninakulilia wewe.+ Njoo haraka unisaidie.+ Sikiliza ninapokulilia.+   Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+Mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama toleo la jioni la nafaka.+   Weka mlinzi wa kinywa changu, Ee Yehova,Weka ulinzi kwenye mlango wa midomo yangu.+   Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote ovu,+Nisishirikiane na watu waovu kutenda mambo mapotovu;Nisile kamwe vyakula vyao vitamu.   Mwadilifu akinipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mshikamanifu;+Akinikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+Ambayo kichwa changu hakiwezi kamwe kukataa.+ Nitaendelea kusali hata wanapopatwa na misiba.   Ingawa waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye jabali,Watu watayasikiliza maneno yangu, kwa maana yanapendeza.   Kama mtu anavyolima na kuuvunja-vunja udongo,Ndivyo mifupa yetu ilivyotawanywa kwenye mlango wa Kaburi.*   Lakini macho yangu yanakutazama wewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ Nimekukimbilia wewe. Usiniue.*   Nilinde dhidi ya mataya ya mtego walionitegea,Dhidi ya mitego ya watenda maovu. 10  Waovu wote wataanguka pamoja ndani ya nyavu zao wenyewe+Huku nikipitia karibu nazo kwa usalama.

Maelezo ya Chini

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Usiimwage chini nafsi yangu.”