Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 17

Biblia Inawezaje Kuisaidia Familia Yako?

WAUME/BABA

“Vivyo hivyo, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Mwanamume anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake, bali huulisha na kuutunza . . . Kila mtu kati yenu anapaswa kumpenda mke wake kama anavyojipenda mwenyewe.”

Waefeso 5:​28, 29, 33

“Nanyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na maagizo ya Yehova.”

Waefeso 6:4

WAKE

“Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”

Waefeso 5:​33

“Enyi wake, jitiisheni kwa waume zenu, kwa kuwa inafaa katika Bwana.”

Wakolosai 3:​18

WATOTO

“Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika muungano na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu. ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’ hiyo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.’”

Waefeso 6:​1-3

“Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo humpendeza Bwana.”

Wakolosai 3:​20