Zaburi 92:1-15
Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato.
92 Ni vema kukushukuru, Ee Yehova+Na kuliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi,
2 Kutangaza upendo wako mshikamanifu+ asubuhiNa uaminifu wako nyakati za usiku,
3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,Kwa sauti tamu ya kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapaza sauti kwa shangwe.
5 Jinsi kazi zako zilivyo kuu, Ee Yehova!+
Jinsi mawazo yako yalivyo na kina sana!+
6 Mtu yeyote asiyetumia akili hawezi kuyajua;Na hakuna mtu yeyote mjinga anayeweza kuelewa hili:+
7 Waovu wanapochipuka kama magugu*Na watenda mabaya wote wanapositawi,Ni ili waangamizwe milele.+
8 Lakini wewe umekwezwa milele, Ee Yehova.
9 Kwa kweli, watazame maadui wako wakishindwa, Ee Yehova,Tazama jinsi maadui wako watakavyoangamia;Watenda maovu wote watatawanywa.+
10 Lakini utazikweza nguvu zangu kama za* fahali mwitu;Nitailainisha ngozi yangu kwa mafuta mapya.+
11 Macho yangu yatawaangalia maadui wangu wakishindwa;+Masikio yangu yatasikia kuhusu kuangamia kwa watu waovu wanaonishambulia.
12 Lakini waadilifu watasitawi kama mtendeNa kuwa wakubwa kama mwerezi kule Lebanoni.+
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;Wanasitawi katika nyua za Mungu wetu.+
14 Hata wakati wa uzeeni* wataendelea kunawiri;+Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+
15 Wakitangaza kwamba Yehova ni mnyoofu.
Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa uadilifu.
Maelezo ya Chini
^ Au “kulipigia muziki.”
^ Au “majani.”
^ Tnn., “utaikweza pembe yangu kama ya.”
^ Au “wakiwa na mvi.”
^ Tnn., “kuwa wanene.”