Zaburi 23:1-6
Muziki wa Daudi.
23 Yehova ni Mchungaji wangu.+
Sitakosa chochote.+
2 Hunilaza katika malisho yenye majani mengi;Huniongoza kwenye sehemu za kupumzika zenye maji mengi.*+
3 Huniburudisha.*+
Huniongoza katika njia za* uadilifu kwa ajili ya jina lake.+
4 Hata nikitembea katika bonde lenye kivuli kizito,+Siogopi madhara yoyote,+Kwa maana wewe uko pamoja nami;+Fimbo yako na gongo lako hunipa uhakika.*
5 Wewe huniandalia meza mbele ya maadui wangu.+
Unakiburudisha* kichwa changu kwa mafuta;+Kikombe changu kimejazwa vizuri.+
6 Kwa hakika wema na upendo mshikamanifu utanifuatia sikuzote za maisha yangu,+Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+
Maelezo ya Chini
^ Au labda, “maji matulivu.”
^ Au “Huiburudisha nafsi yangu.”
^ Tnn., “mapito ya; vijia vya.”
^ Au “hunifariji.”
^ Au “Unakipaka.”