Zaburi 26:1-12
Wa Daudi.
26 Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu;+Nimemtumaini Yehova bila kuyumbayumba.+
2 Nichunguze, Ee Yehova, na unijaribu;Safisha mawazo yangu ya ndani kabisa* na pia moyo wangu.+
3 Kwa maana upendo wako mshikamanifu uko mbele yangu daima,Nami ninatembea katika kweli yako.+
4 Sishirikiani* na watu wadanganyifu,+Nami huwaepuka wale wanaoficha jinsi walivyo.*
5 Ninachukia kundi la waovu,+Nami ninakataa kushirikiana* na waovu.+
6 Nitanawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia,Nami nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu yako, Ee Yehova,
7 Ili niifanye sauti ya utoaji shukrani isikike+Na kutangaza kazi zako zote zinazostaajabisha.
8 Yehova, ninaipenda nyumba ambamo unakaa,+Mahali ambapo utukufu wako hukaa.+
9 Usinifagilie mbali* pamoja na watenda dhambi+Wala kuniua pamoja na watu wakatili,*
10 Ambao mikono yao hutenda matendo ya* aibu,Na ambao mkono wao wa kulia umejaa rushwa.
11 Lakini mimi, nitatembea katika utimilifu wangu.
Niokoe* na kunionyesha kibali.
12 Mguu wangu umesimama mahali tambarare;+Katika kutaniko kubwa,* nitamsifu Yehova.+
Maelezo ya Chini
^ Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
^ Tnn., “Siketi.”
^ Au “sichangamani na wanafiki.”
^ Tnn., “kuketi.”
^ Tnn., “Usiifagilie mbali nafsi yangu.”
^ Au “watu wanaomwaga damu.”
^ Au “mwenendo wa.”
^ Tnn., “Nikomboe.”
^ Tnn., “makusanyiko.”