Zaburi 111:1-10
111 Msifuni Yah!*+
א [Aleph]
Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+ב [Beth]
Katika kikundi kilichokusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko.
ג [Gimel]
2 Kazi za Yehova ni kuu;+ד [Daleth]
Wale wote wanaopendezwa nazo hujifunza kuzihusu.+
ה [He]
3 Utendaji wake ni wenye utukufu na fahari,ו [Waw]
Na uadilifu wake unadumu milele.+
ז [Zayin]
4 Hufanya kazi zake zinazostaajabisha zikumbukwe.+
ח [Heth]
Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+
ט [Teth]
5 Huwapa chakula wale wanaomwogopa.+
י [Yod]
Hukumbuka agano lake milele.+
כ [Kaph]
6 Amewafunulia watu wake kazi zake zenye nguvuל [Lamed]
Kwa kuwapa urithi wa mataifa.+
מ [Mem]
7 Kazi za mikono yake ni kweli na haki;+נ [Nun]
Maagizo yake yote yanategemeka.+
ס [Samekh]
8 Yanategemeka* sikuzote, sasa na milele;ע [Ayin]
Msingi wake ni kweli na uadilifu.+
פ [Pe]
9 Amewakomboa watu wake.+
צ [Tsade]
Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele.
ק [Qoph]
Jina lake ni takatifu na linaogopesha.+
ר [Resh]
10 Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+
ש [Sin]
Wale wote wanaotii maagizo yake wana ufahamu mzuri.+
ת [Taw]
Sifa yake hudumu milele.
Maelezo ya Chini
^ Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
^ Au “neema.”
^ Au “Yana msingi mzuri.”