Zaburi 111:1-10

  • Msifuni Yehova kwa sababu ya kazi zake kuu

    • Jina la Mungu ni takatifu na linaogopesha (9)

    • Kumwogopa Yehova ni hekima (10)

111  Msifuni Yah!*+ א [Aleph] Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+ב [Beth] Katika kikundi kilichokusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko. ג [Gimel]   Kazi za Yehova ni kuu;+ד [Daleth] Wale wote wanaopendezwa nazo hujifunza kuzihusu.+ ה [He]   Utendaji wake ni wenye utukufu na fahari,ו [Waw] Na uadilifu wake unadumu milele.+ ז [Zayin]   Hufanya kazi zake zinazostaajabisha zikumbukwe.+ ח [Heth] Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+ ט [Teth]   Huwapa chakula wale wanaomwogopa.+ י [Yod] Hukumbuka agano lake milele.+ כ [Kaph]   Amewafunulia watu wake kazi zake zenye nguvuל [Lamed] Kwa kuwapa urithi wa mataifa.+ מ [Mem]   Kazi za mikono yake ni kweli na haki;+נ [Nun] Maagizo yake yote yanategemeka.+ ס [Samekh]   Yanategemeka* sikuzote, sasa na milele;ע [Ayin] Msingi wake ni kweli na uadilifu.+ פ [Pe]   Amewakomboa watu wake.+ צ [Tsade] Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele. ק [Qoph] Jina lake ni takatifu na linaogopesha.+ ר [Resh] 10  Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+ ש [Sin] Wale wote wanaotii maagizo yake wana ufahamu mzuri.+ ת [Taw] Sifa yake hudumu milele.

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “neema.”
Au “Yana msingi mzuri.”