Zaburi 136:1-26
136 Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+
2 Mshukuruni Mungu wa miungu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
4 Yeye peke yake ndiye anayetenda mambo makuu yanayostaajabisha,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+
5 Aliziumba mbingu kwa ustadi,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
6 Aliitandaza dunia juu ya maji,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
7 Aliiumba ile mianga mikubwa,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
8 Jua litawale mchana,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
9 Mwezi na nyota zitawale usiku,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
10 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
11 Aliwatoa Waisraeli kutoka kati yao,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
12 Kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
13 Aliigawa Bahari Nyekundu sehemu mbili,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
14 Aliwavusha Waisraeli katikati yake,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
15 Alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
16 Aliwaongoza watu wake kupitia nyikani,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
17 Aliwaua wafalme wakuu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
18 Aliwaua wafalme hodari,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
19 Sihoni+ mfalme wa Waamori,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,
20 Na Ogu+ mfalme wa Bashani,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
21 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
23 Alitukumbuka tulipokuwa wanyonge,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+
24 Alituokoa tena na tena kutoka kwa maadui wetu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
25 Huwapa chakula viumbe wote walio hai,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.