Zaburi 73:1-28
Muziki wa Asafu.+
73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+
2 Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kukengeuka;Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+
3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kiburi*Nilipokuwa nikiona amani ya waovu.+
4 Kwa maana hawana maumivu wanapokufa;Miili yao ina afya.*+
5 Hawataabiki kama wanadamu wengine,+Wala hawateseki kama watu wengine.+
6 Kwa hiyo, kiburi ni mkufu wao;+Ukatili huwafunika kama vazi.
7 Ufanisi wao* hufanya macho yao yanenepe;Wamezidi mawazo ya moyo.
8 Wanadhihaki na kusema mambo maovu.+
Kwa kiburi, wanatoa vitisho vya kuwakandamiza wengine.+
9 Wanaongea kana kwamba wako juu kama mbingu,Na ndimi zao hutamba duniani.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia,Nao hunywa maji yao mengi.
11 Wanasema: “Mungu anajuaje?+
Je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi kweli?”
12 Naam, hivyo ndivyo walivyo waovu, ambao sikuzote wanastarehe.+
Wanaendelea kuongeza mali zao.+
13 Kwa hakika nimeusafisha moyo wangu bureNa kunawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia.+
14 Nami nilitaabika mchana kutwa;+Niliadhibiwa kila asubuhi.+
15 Lakini kama ningesema mambo hayo,Ningewasaliti watu wako.*
16 Nilipojaribu kulielewa jambo hilo,Lilinitaabisha
17 Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu penye utukufu,Nami nikatambua wakati wao ujao.
18 Kwa hakika unawaweka kwenye ardhi yenye utelezi.+
Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+
19 Jinsi wanavyoangamizwa kwa ghafla!+
Jinsi wanavyofikia kwa ghafla mwisho wao unaotisha!
20 Kama ndoto wakati wa kuamka, Ee Yehova,Utakapoinuka, utaitupilia mbali* sanamu yao.
21 Lakini moyo wangu ulikuwa mchungu,+Na ndani kabisa* nilihisi maumivu makali.
22 Nilikuwa mpumbavu wala sikuwa na uelewaji;Nilikuwa kama mnyama asiye na akili mbele zako.
23 Lakini sasa niko pamoja nawe sikuzote;Umeushika mkono wangu wa kulia.+
24 Unaniongoza kwa ushauri wako,+Na baadaye utaniongoza kwenye utukufu.+
25 Ni nani niliye naye mbinguni?
Isipokuwa wewe tu, sitamani chochote duniani.+
26 Mwili wangu na moyo wangu unaweza kudhoofika,Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+
27 Kwa kweli, wale wanaojitenga mbali nawe wataangamia.
Utamwangamiza* kila mtu anayekuacha kwa upotovu.*+
28 Lakini kwa upande wangu, kumkaribia Mungu ni jambo jema kwangu.+
Nimemfanya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kuwa kimbilio langu,Ili nizitangaze kazi zako zote.+
Maelezo ya Chini
^ Au “wanaojigamba.”
^ Au “Kitambi chao kimenenepa.”
^ Tnn., “Mafuta yao.”
^ Tnn., “Ningekisaliti kizazi cha wana wako.”
^ Tnn., “utaidharau.”
^ Tnn., “katika figo zangu.”
^ Tnn., “Utamnyamazisha.”
^ Au “kukosa uaminifu.”