Zaburi 147:1-20
147 Msifuni Yah!*
Ni vema kumwimbia sifa* Mungu wetu;Jinsi inavyopendeza na jinsi inavyofaa sana kumsifu yeye!+
2 Yehova analijenga Yerusalemu;+Huwakusanya pamoja watu wa Israeli waliotawanywa.+
3 Huwaponya waliovunjika moyo;Huyafunga majeraha yao.
4 Huhesabu idadi ya nyota;Zote anaziita kwa majina.+
5 Bwana wetu ni mkuu naye ana nguvu nyingi;+Uelewaji wake haupimiki.+
6 Yehova huwainua wapole,+Lakini huwatupa chini waovu.
7 Mwimbieni Yehova kwa shukrani;Mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi,
8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,Yeye anayeiletea dunia mvua,+Yeye anayechipusha majani+ milimani.
9 Anawapa wanyama chakula,+Kunguru wachanga wanaokililia.+
10 Hapendezwi na nguvu za farasi;+Wala havutiwi na miguu yenye nguvu ya mwanamume.+
11 Yehova anafurahishwa na wale wanaomwogopa,+Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu.+
12 Mtukuze Yehova, Ee Yerusalemu.
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
13 Huyafanya makomeo ya malango ya jiji lako yawe imara;Huwabariki wana wako walio ndani yako.
14 Huleta amani katika eneo lako;+Hukushibisha kwa ngano bora kabisa.*+
15 Huituma amri yake duniani;Neno lake hukimbia upesi sana.
16 Hutoa theluji kama sufu;+Hutawanya theluji nyembamba kama majivu tu.+
17 Huyatupa chini mawe yake ya mvua* kama chembe za mkate.+
Ni nani anayeweza kustahimili baridi yake?+
18 Hulituma neno lake, nayo inayeyuka.
Huufanya upepo wake uvume,+ maji yanatiririka.
19 Anamtangazia Yakobo neno lake,Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+
20 Hajalifanyia hivyo taifa lingine lolote;+Hawajui lolote kuhusu hukumu zake.
Msifuni Yah!*+
Maelezo ya Chini
^ Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
^ Au “kumpigia muziki.”
^ Tnn., “mafuta ya ngano.”
^ Au “Huitupa chini barafu yake.”
^ Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.