Zaburi 38:1-22
Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.
38 Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+
2 Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,Na mkono wako unanikandamiza chini.+
3 Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali.
Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+
4 Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.
5 Vidonda vyangu vinanuka na vina usahaKwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.
7 Ninaungua ndani ya mwili wangu;*Mwili wangu wote ni mgonjwa.+
8 Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*
9 Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako.
10 Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,Na nuru ya macho yangu imetoweka.+
11 Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali.
12 Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+Wananong’onezana uwongo mchana kutwa.
13 Lakini kama kiziwi, sikuwasikiliza;+Na kama bubu, sikufumbua kinywa changu.+
14 Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea.
15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+Nawe ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+
16 Kwa maana nilisema: “Acha wasinichekeWala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.”
17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+
18 Niliungama kosa langu;+Nilihangaishwa na dhambi yangu.+
19 Lakini maadui wangu wana juhudi* na ni hodari,*Wale wanaonichukia bila sababu wameongezeka sana.
20 Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema.
21 Usiniache, Ee Yehova.
Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+
22 Njoo haraka unisaidie,Ee Yehova, wokovu wangu.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
^ Au “ningurume.”
^ Au “nafsi yangu.”
^ Tnn., “wako hai.”
^ Au labda, “Lakini wale ambao ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”