Zaburi 98:1-9
-
Yehova ni Mwokozi na Mwamuzi mwadilifu
-
Wokovu wa Yehova watangazwa (2, 3)
-
Muziki.
98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+Kwa maana ametenda mambo yanayostaajabisha.+
Mkono wake wa kuume, mkono wake mtakatifu, umeleta wokovu.*+
2 Yehova ameutangaza wokovu wake;+Amefunua uadilifu wake mbele ya mataifa.+
3 Amekumbuka upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeona wokovu kutoka kwa* Mungu wetu.+
4 Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.
Changamkeni na kupaza sauti kwa shangwe na kuimba sifa.*+
5 Mwimbieni sifa* Yehova kwa kinubi,Kwa kinubi na wimbo mtamu.
6 Kwa tarumbeta na mlio wa pembe,+Pazeni sauti kwa ushindi mbele za Mfalme, Yehova.
7 Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza,Dunia na wote wanaokaa humo.
8 Mito na ipige makofi;Milima na ipaze sauti pamoja kwa shangwe+
9 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja* kuihukumu dunia.
Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+Na mataifa kwa haki.+
Maelezo ya Chini
^ Au “umemletea ushindi.”
^ Au “ushindi wa.”
^ Au “kupiga muziki.”
^ Au “Mpigieni muziki.”
^ Au “amekuja.”