Zaburi 30:1-12
-
Maombolezo yabadilishwa kuwa shangwe
-
Kibali cha Mungu hudumu maisha yote (5)
-
Muziki. Wimbo wa kuizindua nyumba. Wa Daudi.
30 Nitakukweza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu;Hukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+
3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka Kaburini.*+
Ulifanya niendelee kuwa hai; uliniokoa nisizame shimoni.*+
4 Mwimbieni sifa* Yehova, enyi washikamanifu wake,+Lishukuruni jina lake takatifu;*+
5 Kwa sababu hasira yake ni ya muda mfupi tu,+Lakini kibali chake* hudumu maisha yote.+
Huenda kukawa na kilio jioni, lakini asubuhi, kuna kilio cha shangwe.+
6 Nilipokuwa na amani, nilisema:
“Sitatikiswa kamwe.”*
7 Ee Yehova, nilipokuwa na kibali chako,* ulinifanya niwe imara kama mlima.+
Lakini ulipouficha uso wako, niliogopa.+
8 Niliendelea kukulilia wewe, Ee Yehova;+Nami niliendelea kukusihi wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali.
9 Kuna faida gani nikifa,* nikishuka shimoni?*+
Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yatasimulia kuhusu uaminifu wako?+
10 Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe kibali.+
Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+
11 Umebadili maombolezo yangu kuwa dansi;Umenivua nguo zangu za magunia, nawe unanivisha shangwe,
12 Ili niimbe* sifa yako, nisinyamaze.
Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.
Maelezo ya Chini
^ Au “umenivuta.”
^ Au “umeiinua nafsi yangu.”
^ Au “kaburini.”
^ Au “Mpigieni muziki.”
^ Tnn., “Ushukuruni ukumbusho wake.”
^ Au “nia yake njema.”
^ Au “Sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”
^ Au “nia yako njema.”
^ Tnn., “Damu yangu ina faida gani.”
^ Au “kaburini.”
^ Au “Ili utukufu wangu uimbe.”