Zaburi 17:1-15
Sala ya Daudi.
17 Sikia sihi yangu ya kuomba haki, Ee Yehova;Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada;Sikiliza sala yangu ninayosema bila udanganyifu.+
2 Nawe ufanye uamuzi wa haki kwa niaba yangu;+Macho yako na yaone yaliyo sawa.
3 Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+Umenisafisha;+Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,Na kinywa changu hakijatenda dhambi.
4 Kuhusiana na shughuli za wanadamu,Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za mnyang’anyi.+
5 Acha hatua zangu zibaki kwenye njia zakoIli miguu yangu isijikwae.+
6 Ninakuita wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu.
Nitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+
7 Onyesha upendo wako mshikamanifu kwa njia yenye kustaajabisha,+Ee Mwokozi wa wale wanaokimbilia mkono wako wa kuumeKutoka kwa wale wanaokuasi.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako;+Nifiche katika kivuli cha mabawa yako.+
9 Nilinde kutokana na waovu wanaonishambulia,Kutokana na maadui wangu* wanaoweza kufa ambao wananizingira.+
10 Wamekufa ganzi;*Kwa kinywa chao wanaongea kwa kiburi;
11 Sasa wanatuzingira;+Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.*
12 Yeye ni kama simba anayetamani kurarua windo lake vipandevipande,Kama mwanasimba anayenyemelea mafichoni.
13 Inuka, Ee Yehova, ukabiliane naye+ na kumwangusha chini;Niokoe* kutoka kwa mwovu kwa kutumia upanga wako;
14 Niokoe kwa mkono wako, Ee Yehova,Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* ambao fungu lao liko katika maisha haya,+Wale ambao unawajaza kwa vitu vizuri unavyoandaa+Na ambao huwaachia urithi wana wao wengi.
15 Lakini mimi, nitauona uso wako kwa sababu ya uadilifu wangu;Ninaridhika kuamka mbele zako.*+
Maelezo ya Chini
^ Au “Inama chini na unisikilize.”
^ Au “maadui wangu walio dhidi ya nafsi.”
^ Au “Wamefunikwa na mafuta yao wenyewe.”
^ Au “kututupa chini.”
^ Au “Iokoe nafsi yangu.”
^ Au “mfumo huu wa mambo.”
^ Au “kuona sura yako.”