Zaburi 40:1-17
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
40 Nilimtumaini Yehova kwa bidii,*Naye akanitegea sikio lake na kusikia* kilio changu cha kuomba msaada.+
2 Akanipandisha kutoka katika shimo linalonguruma,Kutoka katika matope yenye utelezi.
Akaiweka miguu yangu juu ya jabali;Akanifanya nisimame mahali palipo imara.
3 Kisha akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,+Asifiwe Mungu wetu.
Wengi watatazama kwa hofuNa kumtumaini Yehova.
4 Mwenye furaha ni mtu anayemtumaini YehovaNa ambaye hawatumaini wakaidi au watu wadanganyifu.*
5 Jinsi ulivyotenda mambo mengi sana,Ee Yehova Mungu wangu,Kazi zako zinazostaajabisha na mawazo yako kutuelekea.+
Hakuna yeyote anayeweza kulinganishwa nawe;+Ikiwa ningejaribu kusimulia na kuongea kuzihusu,Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+
6 Hukutamani* dhabihu na toleo,+Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+
Hukuomba dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.+
7 Kisha nikasema: “Tazama, nimekuja.
Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu.+
8 Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+Na sheria yako imo ndani yangu kabisa.+
9 Ninatangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+
Tazama! Siizuii midomo yangu,+Ee Yehova, kama unavyojua vema.
10 Siufuniki uadilifu wako moyoni mwangu.
Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.
Siufichi upendo wako mshikamanifu na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+
11 Ee Yehova, usininyime rehema yako.
Upendo wako mshikamanifu na ukweli wako na unilinde daima.+
12 Misiba inayonizunguka ni mingi sana haihesabiki.+
Makosa yangu mengi yananilemea hivi kwamba siwezi kuona njia yangu;+Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,Nami nimevunjika moyo.
13 Tafadhali, Ee Yehova, uwe tayari kuniokoa.+
Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+
14 Wote wanaotaka kuniua*Na waaibishwe na kufedheheshwa.
Wale wanaofurahia msiba wanguNa wakimbie kwa aibu.
15 Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”
Na washtuke kwa sababu ya aibu yao.
16 Lakini acha wale wanaokutafuta+Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+
Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:
“Yehova na atukuzwe.”+
17 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;Yehova na anitunze.
Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu;+Mungu wangu, usikawie.+
Maelezo ya Chini
^ Au “Nilimngojea Yehova kwa subira.”
^ Au “akainama chini ili kunisikiliza, akasikia.”
^ Au “waongo.”
^ Au “Hukupendezwa na.”
^ Au “ninatamani.”
^ Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”