Zaburi 52:1-9
Kwa kiongozi. Maskili.* Wa Daudi, Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+
52 Kwa nini unajigamba kuhusu matendo yako maovu, ewe mwenye nguvu?+
Upendo mshikamanifu wa Mungu unadumu mchana kutwa.+
2 Ulimi wako, wenye makali kama wembe,+Hupanga madhara na kutunga mambo ya udanganyifu.+
3 Unapenda uovu kuliko mema,Kusema uwongo kuliko kusema ukweli. (Sela)
4 Unapenda kila neno linalodhuru,Ewe ulimi mdanganyifu!
5 Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+Atakunyakua na kukurarua kutoka katika hema lako;+Atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ (Sela)
6 Waadilifu wataona jambo hilo na kujawa na woga,+Nao watamcheka.+
7 “Huyu ndiye mwanamume ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+Lakini aliutumaini utajiri wake mwingi+Na kutegemea* njama zake mwenyewe za uovu.”*
8 Lakini mimi nitakuwa kama mzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;Ninautumaini upendo mshikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.
9 Nitakusifu milele kwa sababu umechukua hatua;+Mbele ya washikamanifu wako,Nitalitumaini jina lako,+ kwa maana ni jema.