Zaburi 25:1-22
Wa Daudi.
א [Aleph]
25 Nakugeukia wewe,* Ee Yehova.
ב [Beth]
2 Mungu wangu, ninakutumaini wewe;+Usiruhusu niaibishwe.+
Usiruhusu maadui wangu wanicheke.+
ג [Gimel]
3 Kwa hakika hakuna yeyote anayekutumaini atakayeaibishwa,+Lakini aibu inawangoja wale wanaotenda kwa hila bila sababu.+
ד [Daleth]
4 Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+Nifundishe vijia vyako.+
ה [He]
5 Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+Kwa maana wewe ni Mungu wa wokovu wangu.
ו [Waw]
Ninakutumaini mchana kutwa.
ז [Zayin]
6 Kumbuka rehema zako, Ee Yehova, na upendo wako mshikamanifu,+Ambazo umedhihirisha sikuzote.*+
ח [Heth]
7 Usikumbuke dhambi na makosa niliyotenda nilipokuwa kijana.
Nikumbuke kulingana na upendo wako mshikamanifu,+Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+
ט [Teth]
8 Yehova ni mwema na mnyoofu.+
Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda dhambi njia wanayopaswa kuishi.+
י [Yod]
9 Atawaongoza wapole katika yaliyo sawa,*+Naye atawafundisha wapole njia yake.+
כ [Kaph]
10 Njia zote za Yehova ni upendo mshikamanifu na uaminifuKwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+
ל [Lamed]
11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+Nisamehe kosa langu, ingawa ni kubwa.
מ [Mem]
12 Ni nani anayemwogopa Yehova?+
Atamfundisha kuhusu njia anayopaswa kuchagua.+
נ [Nun]
13 Atajionea* yaliyo mema,+Na wazao wake wataimiliki* dunia.+
ס [Samekh]
14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+Naye huwajulisha agano lake.+
ע [Ayin]
15 Macho yangu humtazama Yehova daima,+Kwa maana ataiweka huru miguu yangu kutoka katika wavu.+
פ [Pe]
16 Nielekezee uso wako na kunionyesha kibali,Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo.
צ [Tsade]
17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+Niondolee maumivu yangu makali.
ר [Resh]
18 Yaone mateso yangu na shida yangu,+Nawe unisamehe dhambi zangu zote.+
19 Tazama jinsi maadui wangu walivyo wengiNa jinsi wanavyonichukia vikali.
ש [Shin]
20 Ulinde uhai wangu* na uniokoe.+
Usiruhusu niaibishwe, kwa maana nimekukimbilia wewe.
ת [Taw]
21 Utimilifu na unyoofu na vinilinde,+Kwa maana ninakutumaini wewe.+
22 Ee Mungu, mwokoe* Israeli kutoka katika taabu zake zote.
Maelezo ya Chini
^ Au “Nainua nafsi yangu kwako.”
^ Au “Ambazo ni za tangu nyakati za kale.”
^ Tnn., “katika hukumu.”
^ Au “Nafsi yake itajionea.”
^ Tnn., “mbegu yake itamiliki.”
^ Au “Ilinde nafsi yangu.”
^ Tnn., “mkomboe.”