Zaburi 140:1-13
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
140 Niokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;Nilinde kutoka kwa watu wakatili,+
2 Wale wanaopanga njama za uovu mioyoni mwao+Na kuchochea vita mchana kutwa.
3 Wanaunoa ulimi wao kama wa nyoka;+Sumu ya nyoka vipiri iko nyuma ya midomo yao.+ (Sela)
4 Nilinde, Ee Yehova, kutoka mikononi mwa waovu;+Nilinde kutoka kwa watu wakatili,Wale wanaopanga njama ya kunitega miguu.
5 Wenye kiburi huuficha mtego ili uninase;Kwa kamba wanautandaza wavu kando ya njia.+
Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)
6 Ninamwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.
Sikiliza, Ee Yehova, sihi zangu za kuomba msaada.”+
7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mwokozi wangu mwenye nguvu,Wewe hukinga kichwa changu katika siku ya vita.+
8 Ee Yehova, usitosheleze tamaa za waovu.
Usiruhusu njama zao zifanikiwe, ili wasijikweze. (Sela)+
9 Vichwa vya wale wanaonizingiraNa vifunikwe na uovu unaosemwa na midomo yao.+
10 Makaa ya mawe yanayowaka na yawanyeshee kama mvua.+
Na watupwe motoni,Ndani ya mashimo yenye kina,*+ wasiinuke tena kamwe.
11 Mchongezi na asipate makao duniani.*+
Uovu na uwafuatie watu wakatili na kuwaangamiza.
12 Ninajua kwamba Yehova atawatetea watu wa hali ya chiniNa kuwatendea haki maskini.+
13 Hakika waadilifu watalishukuru jina lako;Wanyoofu watakaa mbele za uso wako.*+