Zaburi 132:1-18
Wimbo wa Safari za Kupanda.
132 Ee Yehova, mkumbuke DaudiNa mateso yake yote;+
2 Jinsi alivyomwapia Yehova,Jinsi alivyomwekea nadhiri hii Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema langu, nyumbani mwangu.+
Sitalala kwenye kochi langu, kitandani mwangu;
4 Sitayaruhusu macho yangu yalale usingizi,Wala kope zangu kusinzia
5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,Makao bora* kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+
6 Tazama! Tulisikia habari hizo huko Efratha;+Tulizipata katika mashamba yaliyo msituni.+
7 Na tuingie katika makao yake;*+Na tuiname chini kwenye kiti cha miguu yake.+
8 Inuka, Ee Yehova, uje mahali pako pa kupumzikia,+Wewe na Sanduku la nguvu zako.+
9 Makuhani wako na wavae uadilifu,Washikamanifu wako na wapaze sauti kwa shangwe.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,Usimkatae* mtiwa-mafuta wako.+
11 Yehova amemwapia Daudi;Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake:
“Mmoja wa wazao wako,*Nitamfanya aketi kwenye kiti chako cha ufalme.+
12 Wana wako wakilishika agano languNa vikumbusho vyangu ninavyowafundisha,+Wana wao piaWataketi kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+
13 Kwa maana Yehova amelichagua Sayuni;+Amelitamani liwe makao yake:+
14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzikia milele;Nitakaa hapa,+ kwa maana nimepatamani.
15 Nitapabariki sana kwa vyakula;Nitawashibisha maskini wake kwa mikate.+
16 Makuhani wake nitawavisha wokovu,+Na washikamanifu wake watapaza sauti kwa shangwe.+
17 Huko nitazifanya nguvu za Daudi zikue.*
Nimemtayarishia taa mtiwa-mafuta wangu.+
18 Nitawavisha aibu maadui wake,Lakini taji lililo kwenye kichwa chake litasitawi.”+
Maelezo ya Chini
^ Au “Hema tukufu la ibada.”
^ Au “hema lake tukufu la ibada.”
^ Tnn., “Usiugeuze nyuma uso wa.”
^ Tnn., “Mmoja kutoka katika uzao wa tumbo lako.”
^ Tnn., “nitaifanya pembe ya Daudi ikue.”