SWALI LA 15

Unawezaje Kuwa na Furaha?

“Ni afadhali kula mboga za majani mahali penye upendo kuliko kula ng’ombe dume aliyenoneshwa mahali penye chuki.”

Methali 15:⁠17

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako, ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.”

Isaya 48:⁠17

“Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao.”

Mathayo 5:3

“Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”

Mathayo 22:⁠39

“Kama vile mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo.”

Luka 6:​31

“Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”

Luka 11:⁠28

“Mtu anapokuwa na vitu vingi, uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”

Luka 12:⁠15

“Basi, tukiwa na chakula na mavazi, tutaridhika na vitu hivyo.”

1 Timotheo 6:8

“Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”

Matendo 20:⁠35