Mwanzo 46:1-34

  • Yakobo na watu wa nyumba yake wanahamia Misri (1-7)

  • Majina ya wenye walihamia Misri (8-27)

  • Yosefu na Yakobo wanakutana Gosheni (28-34)

46  Kwa hiyo Israeli akakamata yote yenye alikuwa nayo* na akaondoka. Wakati alifika Beer-sheba,+ akamutolea zabihu Mungu wa Isaka, baba yake.+ 2  Kisha Mungu akazungumuza na Israeli usiku katika maono na kusema: “Yakobo, Yakobo!” naye akajibu: “Mimi huyu!” 3  Akasema: “Mimi ni Mungu wa kweli, Mungu wa baba yako.+ Usiogope kushuka kuenda Misri, kwa maana nitakufanya kuwa taifa kubwa kule.+ 4  Mimi mwenyewe nitashuka pamoja na wewe kule Misri, na mimi mwenyewe nitakurudisha tena kutoka kule,+ na Yosefu ataweka mukono wake juu ya macho yako.”*+ 5  Kisha mambo hayo Yakobo akaondoka Beer-sheba, na wana wa Israeli wakamubeba Yakobo baba yao na watoto wao na bibi zao katika magari ya kukokotwa yenye Farao alikuwa ametuma ili kumubeba Yakobo. 6  Walienda pamoja na mifugo yao na mali zao, zenye walikuwa wamekusanya katika inchi ya Kanaani. Na mwishowe wakaingia katika Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye. 7  Alienda Misri pamoja na wana wake na wajukuu wake wanaume, watoto wake wanamuke na wajukuu wake wanamuke⁠—​uzao wake wote. 8  Sasa haya ndiyo majina ya wana wa Israeli wenye waliingia Misri,+ Yakobo na wana wake: muzaliwa wa kwanza wa Yakobo alikuwa Rubeni.+ 9  Wana wa Rubeni walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ 10  Wana wa Simeoni+ walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli+ mwana wa mwanamuke Mukanaani. 11  Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni, Kohati, na Merari.+ 12  Wana wa Yuda+ walikuwa Eri, Onani, Shela,+ Perezi,+ na Zera.+ Lakini, Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanaani.+ Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+ 13  Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Iobu, na Shimroni.+ 14  Wana wa Zabuloni+ walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli.+ 15  Hao ndio wana wa Lea, wenye alimuzalia Yakobo kule Padan-aramu, na pia Dina binti yake.+ Watoto wake wote wanaume na watoto wake wote wanamuke walikuwa* makumi tatu na tatu (33). 16  Wana wa Gadi+ walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi, na Areli.+ 17  Wana wa Asheri+ walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, Beria, na dada yao alikuwa Sera. Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.+ 18  Hao ndio wana wa Zilpa,+ mwenye Labani alimupatia Lea binti yake. Zilpa alimuzalia Yakobo watu* kumi na sita (16). 19  Wana wa Raheli, bibi ya Yakobo, walikuwa Yosefu+ na Benyamini.+ 20  Katika inchi ya Misri, Asenati+ binti ya Potifera kuhani wa Oni,* alimuzalia Yosefu wana hawa: Manase+ na Efraimu.+ 21  Wana wa Benyamini+ walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera,+ Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu,+ na Ardi.+ 22  Hao ndio wana wenye Raheli alimuzalia Yakobo: wote walikuwa watu* kumi na ine (14). 23  Mwana* wa Dani+ alikuwa Hushimu.+ 24  Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemu.+ 25  Hao ndio wana wa Bilha, mwenye Labani alimupatia Raheli binti yake. Bilha alimuzalia Yakobo hawa: watu* saba (7) kwa ujumla. 26  Wale wote wenye walikuwa* wazao wa Yakobo na wenye waliingia Misri pamoja naye walikuwa makumi sita na sita (66), bila kuhesabu bibi za wana wa Yakobo.+ 27  Wana wa Yosefu wenye walizaliwa katika Misri walikuwa wawili.* Watu wote wa* nyumba ya Yakobo wenye waliingia Misri walikuwa makumi saba (70).+ 28  Yakobo akamutuma Yuda+ atangulie na kumuambia Yosefu kwamba alikuwa katika njia kuenda Gosheni. Wakati waliingia katika inchi ya Gosheni,+ 29  Yosefu akaagiza gari lake litayarishwe na akapanda kuenda kumupokea Israeli baba yake kule Gosheni. Wakati alijitambulisha kwa baba yake, mara moja akamukumbatia* baba yake na kulia kwa wakati fulani.* 30  Kisha Israeli akamuambia Yosefu: “Sasa niko tayari kufa; nimeona uso wako na kujua kwamba ungali muzima.” 31  Kisha Yosefu akaambia ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake: “Muache nipande kuenda kumujulisha Farao+ na kumuambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumba ya baba yangu wenye walikuwa katika inchi ya Kanaani wamekuja hapa kwangu.+ 32  Watu hao ni wachungaji,+ na wanafuga mifugo,+ na wameleta makundi yao na mifugo yao na kila kitu chenye wako nacho.’+ 33  Wakati Farao atawaita na kuwauliza, ‘Munafanya kazi gani?’ 34  munapaswa kusema, ‘Watumishi wako wamefuga mifugo tangu ujana wao mupaka sasa, sisi na mababu zetu,’+ ili muweze kuishi katika inchi ya Gosheni,+ kwa maana kila muchungaji wa kondoo ni chukizo kwa Wamisri.”+

Maelezo ya Chini

Ao “watu wote wenye walikuwa wake.”
Ni kusema, atayafunga wakati Yakobo atakufa.
Ao “Nafsi zote za watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke zilikuwa.”
Ao “nafsi.”
Ni kusema, Heliopolisi.
Ao “nafsi.”
Tnn., “Wana.”
Ao “nafsi.”
Ao “Nafsi zote zenye zilikuwa.”
Ao “nafsi mbili.”
Ao “nafsi zote za.”
Tnn., “akamuangukia kwenye shingo yake.”
Ao “akalia kwenye shingo yake tena na tena.”