Mwanzo 46:1-34
46 Kwa hiyo Israeli akakamata yote yenye alikuwa nayo* na akaondoka. Wakati alifika Beer-sheba,+ akamutolea zabihu Mungu wa Isaka, baba yake.+
2 Kisha Mungu akazungumuza na Israeli usiku katika maono na kusema: “Yakobo, Yakobo!” naye akajibu: “Mimi huyu!”
3 Akasema: “Mimi ni Mungu wa kweli, Mungu wa baba yako.+ Usiogope kushuka kuenda Misri, kwa maana nitakufanya kuwa taifa kubwa kule.+
4 Mimi mwenyewe nitashuka pamoja na wewe kule Misri, na mimi mwenyewe nitakurudisha tena kutoka kule,+ na Yosefu ataweka mukono wake juu ya macho yako.”*+
5 Kisha mambo hayo Yakobo akaondoka Beer-sheba, na wana wa Israeli wakamubeba Yakobo baba yao na watoto wao na bibi zao katika magari ya kukokotwa yenye Farao alikuwa ametuma ili kumubeba Yakobo.
6 Walienda pamoja na mifugo yao na mali zao, zenye walikuwa wamekusanya katika inchi ya Kanaani. Na mwishowe wakaingia katika Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
7 Alienda Misri pamoja na wana wake na wajukuu wake wanaume, watoto wake wanamuke na wajukuu wake wanamuke—uzao wake wote.
8 Sasa haya ndiyo majina ya wana wa Israeli wenye waliingia Misri,+ Yakobo na wana wake: muzaliwa wa kwanza wa Yakobo alikuwa Rubeni.+
9 Wana wa Rubeni walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+
10 Wana wa Simeoni+ walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli+ mwana wa mwanamuke Mukanaani.
11 Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni, Kohati, na Merari.+
12 Wana wa Yuda+ walikuwa Eri, Onani, Shela,+ Perezi,+ na Zera.+ Lakini, Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanaani.+
Wana wa Perezi walikuwa Hezroni na Hamuli.+
13 Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Iobu, na Shimroni.+
14 Wana wa Zabuloni+ walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli.+
15 Hao ndio wana wa Lea, wenye alimuzalia Yakobo kule Padan-aramu, na pia Dina binti yake.+ Watoto wake wote wanaume na watoto wake wote wanamuke walikuwa* makumi tatu na tatu (33).
16 Wana wa Gadi+ walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi, na Areli.+
17 Wana wa Asheri+ walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, Beria, na dada yao alikuwa Sera.
Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.+
18 Hao ndio wana wa Zilpa,+ mwenye Labani alimupatia Lea binti yake. Zilpa alimuzalia Yakobo watu* kumi na sita (16).
19 Wana wa Raheli, bibi ya Yakobo, walikuwa Yosefu+ na Benyamini.+
20 Katika inchi ya Misri, Asenati+ binti ya Potifera kuhani wa Oni,* alimuzalia Yosefu wana hawa: Manase+ na Efraimu.+
21 Wana wa Benyamini+ walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera,+ Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu,+ na Ardi.+
22 Hao ndio wana wenye Raheli alimuzalia Yakobo: wote walikuwa watu* kumi na ine (14).
23 Mwana* wa Dani+ alikuwa Hushimu.+
24 Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemu.+
25 Hao ndio wana wa Bilha, mwenye Labani alimupatia Raheli binti yake. Bilha alimuzalia Yakobo hawa: watu* saba (7) kwa ujumla.
26 Wale wote wenye walikuwa* wazao wa Yakobo na wenye waliingia Misri pamoja naye walikuwa makumi sita na sita (66), bila kuhesabu bibi za wana wa Yakobo.+
27 Wana wa Yosefu wenye walizaliwa katika Misri walikuwa wawili.* Watu wote wa* nyumba ya Yakobo wenye waliingia Misri walikuwa makumi saba (70).+
28 Yakobo akamutuma Yuda+ atangulie na kumuambia Yosefu kwamba alikuwa katika njia kuenda Gosheni. Wakati waliingia katika inchi ya Gosheni,+
29 Yosefu akaagiza gari lake litayarishwe na akapanda kuenda kumupokea Israeli baba yake kule Gosheni. Wakati alijitambulisha kwa baba yake, mara moja akamukumbatia* baba yake na kulia kwa wakati fulani.*
30 Kisha Israeli akamuambia Yosefu: “Sasa niko tayari kufa; nimeona uso wako na kujua kwamba ungali muzima.”
31 Kisha Yosefu akaambia ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake: “Muache nipande kuenda kumujulisha Farao+ na kumuambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumba ya baba yangu wenye walikuwa katika inchi ya Kanaani wamekuja hapa kwangu.+
32 Watu hao ni wachungaji,+ na wanafuga mifugo,+ na wameleta makundi yao na mifugo yao na kila kitu chenye wako nacho.’+
33 Wakati Farao atawaita na kuwauliza, ‘Munafanya kazi gani?’
34 munapaswa kusema, ‘Watumishi wako wamefuga mifugo tangu ujana wao mupaka sasa, sisi na mababu zetu,’+ ili muweze kuishi katika inchi ya Gosheni,+ kwa maana kila muchungaji wa kondoo ni chukizo kwa Wamisri.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “watu wote wenye walikuwa wake.”
^ Ni kusema, atayafunga wakati Yakobo atakufa.
^ Ao “Nafsi zote za watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke zilikuwa.”
^ Ao “nafsi.”
^ Ni kusema, Heliopolisi.
^ Ao “nafsi.”
^ Tnn., “Wana.”
^ Ao “nafsi.”
^ Ao “Nafsi zote zenye zilikuwa.”
^ Ao “nafsi mbili.”
^ Ao “nafsi zote za.”
^ Tnn., “akamuangukia kwenye shingo yake.”
^ Ao “akalia kwenye shingo yake tena na tena.”