Mwanzo 38:1-30
-
Yuda na Tamari (1-30)
38 Wakati huo, Yuda akaacha ndugu zake na kuenda kusimamisha hema yake karibu na mwanaume mumoja Mwadulamu mwenye aliitwa Hira.
2 Yuda akaona kule binti mumoja Mukanaani+ mwenye aliitwa Shua. Kwa hiyo akamukamata na kulala naye,
3 na akakuwa na mimba. Kisha wakati fulani akamuzaa mwana, na Yuda akamupatia jina Eri.+
4 Akakuwa tena na mimba na akazaa mwana na akamupatia jina Onani.
5 Kisha akazaa tena mwana na akamupatia jina Shela. Huyo* alikuwa katika muji wa Akzibu+ wakati Shua alizaa Shela.
6 Kisha wakati fulani, Yuda akamuchukulia Eri muzaliwa wake wa kwanza bibi, na jina lake lilikuwa Tamari.+
7 Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alimuchukiza Yehova; kwa hiyo Yehova akamuua.
8 Basi Yuda akamuambia Onani: “Lala na bibi ya ndugu yako na ufanye ndoa ya mutu na shemeki yake pamoja na Tamari na utokeze uzao kwa ajili ya ndugu yako.”+
9 Lakini Onani alijua kwamba uzao huo haungeonwa kuwa wake.+ Kwa hiyo wakati alilala na bibi ya ndugu yake, alimwanga mbegu zake za uzazi* chini ili asimuinulie ndugu yake uzao.+
10 Jambo lenye alifanya lilikuwa mubaya mbele ya macho ya Yehova, kwa hiyo akamuua pia.+
11 Yuda akamuambia Tamari binti-mukwe wake: “Kaa ukiwa mujane katika nyumba ya baba yako mupaka Shela mwana wangu akomae,” kwa maana Yuda alisema katika moyo wake: ‘Yeye pia anaweza kufa kama vile ndugu zake.’+ Kwa hiyo Tamari akaenda na kuishi katika nyumba ya baba yake.
12 Wakati fulani ukapita, na bibi ya Yuda, binti ya Shua,+ akakufa. Yuda akamaliza kipindi cha kuomboleza, na kisha akaenda Timna+ mahali watu wake wa kukata manyoya ya kondoo walikuwa, alienda kule pamoja na Hira rafiki yake Mwadulamu.+
13 Tamari akaambiwa: “Baba-mukwe wako anapanda kuenda Timna ili kukata manyoya ya kondoo wake.”
14 Basi akatosha nguo zake za ujane na akajifunika uso na pia akajifunika kwa kitambaa kikubwa na akakaa kwenye muingilio wa Enaimu, muji wenye kuwa kwenye barabara ya kuenda Timna, kwa maana aliona kwamba Shela alikuwa amekomaa na bado hakukuwa amepewa kwa Shela ili akuwe bibi yake.+
15 Wakati Yuda alimuona, mara moja akafikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amejifunika uso.
16 Kwa hiyo akapita karibu naye pembeni ya barabara na kumuambia: “Tafazali, uniruhusu, nilale na wewe,” kwa maana hakujua kwamba alikuwa binti-mukwe wake.+ Lakini, Tamari akasema: “Utanipatia nini ili ulale na mimi?”
17 Akasema: “Nitatuma mwana-mbuzi kutoka katika mifugo yangu.” Lakini Tamari akasema: “Utawekesha kitu gani mupaka wakati utatuma mwana-mbuzi huyo?”
18 Yuda akaendelea kusema: “Unapenda nikuwekeshe kitu gani?” akasema: “Pete yako ya kutia muhuri,+ kamba yako na fimbo yenye kuwa katika mukono wako.” Kisha akamupatia vile vitu na akalala naye, na Tamari akakuwa na mimba ya Yuda.
19 Kisha mambo hayo Tamari akasimama na akaenda na kutosha kitambaa chake kikubwa na kuvaa nguo zake za ujane.
20 Na Yuda akatuma mwana-mbuzi kupitia rafiki yake Mwadulamu,+ ili kukamata vitu vyenye aliwekesha katika mukono wa ule mwanamuke, lakini hakumupata.
21 Akauliza watu wa muji huo, kwa kusema: “Iko* wapi ule kahaba wa hekalu katika Enaimu pembeni ya barabara?” Lakini wakasema: “Hakujakuwaka kahaba wa hekalu mahali hapa.”
22 Mwishowe akarudia kwa Yuda na kusema: “Sikumupata, na watu wa mahali pale walisema, ‘Hakujakuwaka kahaba wa hekalu mahali hapa.’”
23 Kwa hiyo Yuda akasema: “Muache avikamate vikuwe vyake, ili watu wasituzarau. Kwa vyovyote, nimetuma huyu mwana-mbuzi, lakini haukumupata.”
24 Lakini, kisha miezi tatu (3) hivi, Yuda aliambiwa: “Tamari binti-mukwe wako amefanya ukahaba, na pia amepata mimba katika ukahaba wake.” Basi Yuda akasema: “Mumutie inje na ateketezwe kwa moto.”+
25 Wakati walikuwa wanamupeleka inje, akatuma ujumbe huu kwa baba-mukwe wake: “Mwanaume mwenye vitu hivi ndiye alinipatia mimba.” Kisha Tamari akaongeza kusema: “Tafazali chunguza uone ni nani mwenye pete hii ya kutia muhuri na kamba hii na fimbo hii.”+
26 Kisha Yuda akachunguza vitu hivyo na kusema: “Yeye ni mwenye haki zaidi kuliko mimi, kwa sababu sikumupatia Shela mwana wangu akuwe bwana yake.”+ Na kisha mambo hayo, Yuda hakufanya ngono naye tena.
27 Wakati muda wake wa kuzaa ulifika, kulikuwa mapacha katika tumbo lake la uzazi.
28 Wakati alikuwa anazaa, mutoto mumoja alitia mukono wake inje, na mara moja mwanamuke wa kuzalisha akakamata uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa na kuifunga kuzunguka mukono wa mutoto huyo, akisema: “Ni huyu alitoka wa kwanza.”
29 Lakini wakati tu alirudisha mukono wake nyuma, ndugu yake akatoka, na mara moja mwanamuke wa kuzalisha akasema: “Mbona umejipasulia njia kwa nguvu!” Kwa hiyo akapewa jina Perezi.*+
30 Kisha ndugu yake akatoka, uzi ya rangi nyekundu yenye kungaa ilikuwa inafungwa kuzunguka mukono wake, na akapewa jina Zera.+
Maelezo ya Chini
^ Ni kusema, Yuda.
^ Ao “shahawa zake.”
^ Ao “Eko.”
^ Maana yake “Mupasuko,” pengine inamaanisha kupasuka kwa musamba. Musamba ni sehemu ya katikati ya mwili yenye inaunganisha mapaja na kiwiliwili.