Mwanzo 20:1-18
-
Sara anaokolewa katika mikono ya Abimeleki (1-18)
20 Sasa Abrahamu akahamisha kambi yake kutoka kule+ mupaka inchi ya Negebu na akaanza kuishi katikati ya Kadeshi+ na Shuri.+ Wakati alikuwa anakaa* Gerari,+
2 Abrahamu akasema tena juu ya Sara bibi yake: “Yeye ni dada yangu.”+ Kwa hiyo Abimeleki mufalme wa Gerari akatuma watu wamulete Sara na akamuchukua.+
3 Kisha, Mungu akamutokea Abimeleki usiku katika ndoto na kumuambia: “Angalia, wewe ni kama tu umekufa kwa sababu ya mwanamuke mwenye ulichukua,+ kwa maana yeye ni mwenye kuolewa na ni bibi ya mwanaume mwingine.”+
4 Lakini, Abimeleki alikuwa hajamukaribia.* Kwa hiyo akasema: “Yehova, je, utaua taifa lenye halina kosa kabisa?*
5 Je, Abrahamu hakuniambia, ‘Yeye ni dada yangu,’ na je, Sara pia hakusema, ‘Yeye ni ndugu yangu’? Nilifanya jambo hilo kwa moyo muzuri na kwa mikono yenye haina kosa.”
6 Basi Mungu wa kweli akamuambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya vile kwa moyo muzuri, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee zambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umuguse.
7 Sasa rudisha bibi ya mwanaume huyo, kwa maana mwanaume huyo ni nabii,+ atamulilia Mungu* kwa ajili yako+ na utaendelea kuishi. Lakini kama haumurudishe, ujue kama hakika utakufa, wewe na watu wote wa nyumba yako.”
8 Abimeleki akaamuka asubui sana na akaita watumishi wake wote na akawaambia mambo hayo yote, nao wakaogopa sana.
9 Kisha Abimeleki akamuita Abrahamu na kumuambia: “Ni jambo gani hili umetutendea? Ni zambi gani nimekutendea ili ulete juu yangu na juu ya ufalme wangu zambi kubwa kama hii? Jambo lenye umenitendea haliko sawa.”
10 Na Abimeleki akaendelea kumuambia Abrahamu: “Ulikuwa na nia gani wakati ulifanya jambo hilo?”+
11 Abrahamu akasema: “Ilikuwa kwa sababu nilisema katika moyo wangu, ‘Hakuna kabisa woga wa Mungu mahali hapa, na wataniua kwa sababu ya bibi yangu.’+
12 Na tena, yeye kwa kweli ni dada yangu, ni binti ya baba yangu lakini haiko binti ya mama yangu, naye akakuwa bibi yangu.+
13 Kwa hiyo wakati Mungu alinifanya nitange-tange mbali na nyumba ya baba yangu,+ nilimuambia Sara: ‘Ni hivi utakuwa unanionyesha upendo mushikamanifu: Kila mahali kwenye tutaenda, sema hivi juu yangu, ‘Yeye ni ndugu yangu.”’”+
14 Basi Abimeleki akakamata kondoo na ngombe na watumishi wanaume na watumishi wanamuke na akamupatia Abrahamu, na Abimeleki akamurudishia Abrahamu bibi yake Sara.
15 Tena Abimeleki akasema: “Angalia, inchi yangu iko mbele yako. Kaa mahali popote kwenye unapenda.”
16 Na akamuambia Sara: “Angalia, ninamupatia ndugu yako vipande elfu moja (1 000) vya feza.+ Ni alama kwa wote wenye kuwa pamoja na wewe na mbele ya kila mutu kwamba hauna kosa, na umeondolewa lawama.”
17 Na Abrahamu akaanza kumulilia* Mungu wa kweli, na Mungu akamuponyesha Abimeleki na bibi yake na watumwa wake wanamuke, nao wakaanza kupata watoto;
18 kwa maana Yehova alikuwa amefanya wanamuke wote wa nyumba ya Abimeleki wakuwe tasa* kwa sababu ya Sara, bibi ya Abrahamu.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “anaishi akiwa mugeni.”
^ Ni kusema, alikuwa hajafanya ngono naye.
^ Ao “lenye haki.”
^ Ao “ataomba dua.”
^ Ao “kuomba dua kwa.”
^ Ao “alikuwa amefunga kabisa kila tumbo la uzazi la nyumba ya Abimeleki.”