Mwanzo 45:1-28

  • Yosefu anajitambulisha (1-15)

  • Ndugu za Yosefu wanaenda kumuchukua Yakobo (16-28)

45  Wakati huo Yosefu hakuweza tena kujizuia mbele ya watumishi wake wote.+ Kwa hiyo akasema kwa sauti kubwa: “Mutoshe kila mutu mbele yangu!” Hakuna mutu mwingine mwenye alibakia pamoja naye wakati Yosefu alijitambulisha mwenyewe kwa ndugu zake.+ 2  Kisha akaanza kulia kwa sauti kubwa mupaka Wamisri wakasikia na nyumba ya Farao ikasikia. 3  Mwishowe Yosefu akaambia ndugu zake: “Mimi ni Yosefu. Je, baba yangu angali muzima?” Lakini ndugu zake hawakuweza kumujibu, kwa maana walishituka sana kwa sababu yake. 4  Kwa hiyo Yosefu akaambia ndugu zake: “Tafazali, munikaribie.” Basi wakamukaribia. Kisha akasema: “Mimi ni Yosefu ndugu yenu, mwenye muliuzisha apelekwe Misri.+ 5  Lakini sasa musihuzunike na kila mumoja asimulaumu mwenzake kwa sababu muliniuzisha huku; kwa sababu Mungu alinituma mbele yenu ili kulinda uzima.+ 6  Huu ni mwaka wa pili wa njaa katika inchi,+ na kungali miaka tano (5) yenye hakutakuwa kulima wala kuvuna. 7  Lakini Mungu alinituma mbele yenu ili kulinda mabaki kwa ajili yenu+ juu ya dunia* na kuwaokoa kwa wokovu mukubwa. 8  Kwa hiyo basi, haiko ninyi ndio mulinituma huku, lakini ni Mungu wa kweli, ili aniweke kuwa mushauri mukubwa* wa Farao na bwana kwa ajili ya nyumba yake yote na mutawala juu ya inchi yote ya Misri.+ 9  “Murudie haraka kwa baba yangu, na munapaswa kumuambia, ‘Mwana wako Yosefu anasema: “Mungu ameniweka kuwa bwana juu ya Misri yote.+ Shuka ukuje kwangu. Usikawie.+ 10  Unapaswa kukaa katika inchi ya Gosheni,+ mahali kwenye utakuwa karibu na mimi⁠—​wewe, wana wako, wajukuu wako, makundi yako, mifugo yako, na kila kitu chenye uko nacho. 11  Nitakupatia chakula kule, kwa maana kungali miaka tano (5) ya njaa.+ Kama haiko vile, utakuwa maskini, wewe na nyumba yako na kila kitu chenye uko nacho.’” 12  Ninyi na ndugu yangu Benyamini munajionea na macho yenu wenyewe kwamba ni mimi ninazungumuza na ninyi.+ 13  Kwa hiyo munapaswa kumuambia baba yangu kuhusu utukufu wangu katika Misri na kila kitu chenye mumeona. Sasa mufanye haraka na mumulete baba yangu hapa.” 14  Kisha akamukumbatia Benyamini ndugu yake na akaanza kulia, na Benyamini akalia na mikono ya Yosefu ilikuwa imezunguka shingo ya Benyamini.+ 15  Na akabusu ndugu zake wote na akalia juu ya shingo zao, na kisha mambo hayo ndugu zake wakazungumuza naye. 16  Habari ikafika katika nyumba ya Farao: “ Ndugu za Yosefu wamekuja!” Habari hiyo ikamufurahisha Farao na watumishi wake. 17  Kwa hiyo Farao akamuambia Yosefu: “Ambia ndugu zako, ‘Mufanye hivi: Mubebeshe wanyama wenu mizigo na muende katika inchi ya Kanaani, 18  na muchukue baba yenu na watu wa nyumba zenu na mukuje hapa kwangu. Nitawapatia vitu vya muzuri vya inchi ya Misri, na mutakula* sehemu yenye utajiri mukubwa zaidi ya* inchi.’+ 19  Na unaamuriwa kuwaambia:+ ‘Mufanye hivi: Mukamate magari ya kukokotwa+ ya inchi ya Misri kwa ajili ya watoto wenu na bibi zenu, na munapaswa kumuleta baba yenu juu ya moja ya magari hayo na kuja hapa.+ 20  Musikuwe na wasiwasi juu ya mali zenu,+ kwa maana vitu vya muzuri zaidi vya inchi ya Misri ni vyenu.’” 21  Na wana wa Israeli wakafanya vile, na Yosefu akawapatia magari ya kukokotwa kama vile Farao aliamuru, na akawapatia chakula kwa ajili ya safari. 22  Akapatia kila mumoja wao nguo za kubadilisha, lakini akamupatia Benyamini vipande mia tatu (300) vya feza na nguo tano (5) za kubadilisha.+ 23  Na akamutumia baba yake vitu hivi: punda kumi (10) wenye kubeba vitu vya muzuri vya Misri na punda-dike kumi wenye kubeba nafaka na mikate na vyakula vingine kwa ajili ya safari ya baba yake. 24  Kwa hiyo akaacha ndugu zake waende, na wakati walikuwa wanaondoka, akawaambia: “Musigombane katika njia.”+ 25  Kisha wakaondoka Misri na kufika katika inchi ya Kanaani kwa Yakobo baba yao. 26  Kisha wakamuambia: “Yosefu angali muzima, na yeye ndiye mutawala juu ya inchi yote ya Misri!”+ Lakini moyo wake haukushituka kabisa kwa sababu hakuwaamini.+ 27  Wakati waliendelea kumuambia maneno yote yenye Yosefu alikuwa amewaambia na wakati aliona magari ya kukokotwa yenye Yosefu alikuwa ametuma ili yamubebe, roho ya Yakobo ikaanza kufufuka. 28  Mara moja Israeli akasema: “Inatosha! Mwana wangu Yosefu angali muzima! Ninapaswa kuenda na kumuona mbele nikufe!”+

Maelezo ya Chini

Ao “katika inchi.”
Tnn., “kama baba.”
Ao “mutaishi kwa kutegemea.”
Ao “unono wa.”