Mwanzo 40:1-23
40 Kisha mambo hayo, mukubwa wa wanyweshaji+ wa mufalme wa Misri na mukubwa wa watengenezaji wa mikate walimutendea zambi bwana wao, mufalme wa Misri.
2 Kwa hiyo Farao akakasirikia wale maofisa wawili, mukubwa wa wanyweshaji na mukubwa wa watengenezaji wa mikate,+
3 na akawatia katika gereza la nyumba ya mukubwa wa walinzi,+ kwenye Yosefu alikuwa amefungwa.+
4 Kisha mukubwa wa walinzi akamupatia Yosefu mugao wa kuwa pamoja nao na kuwahangaikia,+ na wakabakia katika gereza kwa wakati* fulani.
5 Munyweshaji na mutengenezaji wa mikate wa mufalme wa Misri, wenye walikuwa wanafungwa katika gereza, kila mumoja aliota ndoto usiku uleule, na kila ndoto ilikuwa na mafasirio yake.
6 Asubui ya kufuata, wakati Yosefu aliingia na kuwaona, walionekana kuwa wenye huzuni.
7 Kwa hiyo akauliza wale wafanyakazi maofisa wa Farao wenye walikuwa wamefungwa pamoja naye katika nyumba ya bwana wake: “Sababu gani nyuso zenu ziko na huzuni leo?”
8 Basi wakamuambia: “Kila mumoja wetu aliota ndoto, lakini hakuna mutu wa kutufasiria maana yake.” Yosefu akawaambia: “Je, mafasirio hayatoke kwa Mungu?+ Tafazali, munielezee ndoto zenu.”
9 Kwa hiyo mukubwa wa wanyweshaji akamuelezea Yosefu ndoto yake, akamuambia: “Katika ndoto yangu, kulikuwa muzabibu mbele yangu.
10 Na kwenye ule muzabibu, kulikuwa matawi tatu (3), na wakati ulikuwa unatoa machipukizi, ulitoa maua, na mafungu-mafungu yake yakatoa zabibu zenye kuivya.
11 Na kikombe cha Farao kilikuwa katika mukono wangu, na nikakamata zabibu na kuzikamulia ndani ya kikombe cha Farao. Kisha pale nikatia kile kikombe katika mukono wa Farao.”
12 Kisha Yosefu akamuambia: “Haya ndiyo mafasirio yake: yale matawi tatu (3) ni siku tatu.
13 Kisha siku tatu (3), Farao atakutosha katika gereza,* atakurudisha katika kazi yako,+ na utaweka kikombe cha Farao katika mukono wake kama vile ulikuwa unafanya zamani wakati ulikuwa munyweshaji wake.+
14 Lakini, unapaswa kunikumbuka wakati mambo yatakuendea muzuri. Tafazali unionyeshe upendo mushikamanifu na unitaje mbele ya Farao, ili nitoke hapa.
15 Kwa kweli, nilikamatwa katika inchi ya Waebrania,+ na sijafanya hapa jambo lolote lenye linaweza kuacha wanitie katika gereza.”*+
16 Wakati mukubwa wa watengenezaji wa mikate aliona kwamba Yosefu alikuwa amefasiria jambo fulani la muzuri, akamuambia: “Mimi pia nilikuwa katika ndoto yangu, na kulikuwa vitunga tatu (3) vya mikate ya mweupe juu ya kichwa changu,
17 na ndani ya kitunga cha juu, kulikuwa vitu vya muzuri vya kila namna vyenye vilipikwa kwa ajili ya Farao, na kulikuwa ndege wenye walikuwa wanakula vitu hivyo katika kitunga juu ya kichwa changu.
18 Kisha Yosefu akajibu, “Haya ndiyo mafasirio yake: Vile vitunga tatu (3) ni siku tatu.
19 Kisha siku tatu (3), Farao atakukata kichwa na kukutundika kwenye muti, na ndege watakula mwili wako.”+
20 Sasa siku ya tatu (3) ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao,+ na alifanya karamu kwa ajili ya watumishi wake wote, na akatosha katika gereza* mukubwa wa wanyweshaji na mukubwa wa watengenezaji wa mikate mbele ya watumishi wake.
21 Na akamurudisha mukubwa wa wanyweshaji katika kazi yake ya munyweshaji, na akaendelea kumupatia Farao kikombe.
22 Lakini akamutundika mukubwa wa watengenezaji wa mikate, kama vile Yosefu alikuwa amewafasiria.+
23 Hata hivyo, ule mukubwa wa wanyweshaji hakumukumbuka Yosefu; aliendelea kumusahau.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “siku.”
^ Tnn., “atainua kichwa chako.”
^ Tnn., “tangi; shimo.”
^ Tnn., “akainua kichwa cha.”