Mwanzo 33:1-20
33 Sasa Yakobo akainua macho yake na kumuona Esau anakuja, na wanaume mia ine (400) walikuwa pamoja naye.+ Kwa hiyo akagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale watumishi wanamuke wawili.+
2 Akaweka wale watumishi wanamuke na watoto wao mbele,+ kisha Lea na watoto wake,+ na Raheli+ na Yosefu nyuma yao.
3 Kisha yeye mwenyewe akapita mbele yao na kuinama mupaka chini mara saba (7) wakati alimukaribia ndugu yake.
4 Lakini Esau akakimbia ili kukutana naye, akamukumbatia na kumubusu, nao wakaanza kulia.
5 Wakati aliinua macho yake na kuona wanamuke na watoto, akasema: “Ni nani hawa wenye kuwa pamoja na wewe?” Yakobo akamuambia: “Hawa ni watoto wenye Mungu amemupatia mutumishi wako.”+
6 Basi watumishi wanamuke wakaenda mbele pamoja na watoto wao na kuinama chini,
7 na Lea pia akaenda mbele pamoja na watoto wake, nao wakainama chini. Kisha Yosefu akaenda mbele pamoja na Raheli, nao wakainama chini.+
8 Esau akasema: “Kambi yote hii ya wasafiri yenye nimekutana nayo iko na kusudi gani?”+ Yakobo akajibu: “Ili kukubaliwa mbele ya macho ya bwana wangu.”+
9 Kisha Esau akasema: “Niko na mali nyingi sana, ndugu yangu.+ Bakia na mali yako.”
10 Lakini Yakobo akasema: “Hapana, tafazali. Kama nimekubaliwa mbele ya macho yako, unapaswa kukubali zawadi ya mukono wangu, kwa sababu nimeileta ili nione uso wako. Na nimeona uso wako kama vile kuona uso wa Mungu, kwa sababu umenipokea kwa furaha.+
11 Tafazali, kamata zawadi ya baraka yenye ililetwa kwako,+ kwa sababu Mungu amenibariki na niko na kila kitu chenye ninahitaji.”+ Na akaendelea kumukaza, mupaka akaikamata.
12 Kisha wakati fulani Esau akasema: “Tuondoke na tuende, na mimi nikutangulie.”
13 Lakini Yakobo akamuambia: “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wazaifu+ na niko na kondoo na ngombe wenye kunyonyesha vitoto vyao. Ikiwa wanapelekwa haraka-haraka sana kwa siku moja, basi kundi lote litakufa.
14 Tafazali, bwana wangu atangulie mutumishi wake, lakini mimi nitaendelea na safari polepole kwa mwendo wa mifugo na wa watoto mupaka wakati nitafika kwa bwana wangu kule Seiri.”+
15 Kisha Esau akasema: “Tafazali, uniruhusu niache watu wangu fulani pamoja na wewe.” Yakobo akasema, “Sababu gani ufanye vile? Ninaomba tu nikubaliwe mbele ya macho ya bwana wangu.”
16 Basi siku hiyo Esau akasafiri na kurudia Seiri.
17 Na Yakobo akasafiri mupaka Sukoti,+ na akajijengea nyumba na kutengeneza vibanda kwa ajili ya mifugo yake. Ndiyo sababu aliita mahali pale Sukoti.*
18 Kisha kutoka Padan-aramu,+ Yakobo akafika salama kwenye muji wa Shekemu+ katika inchi ya Kanaani,+ na akapiga kambi karibu na ule muji.
19 Kisha akanunua sehemu ya shamba ya wana wa Hamori, baba ya Shekemu, kwa vipande mia moja (100) vya feza,+ akasimamisha hema yake pale.
20 Akasimamisha mazabahu mahali pale na kuipatia jina Mungu, Mungu wa Israeli.+
Maelezo ya Chini
^ Maana yake “Vibanda.”