Mwanzo 16:1-16

  • Hagari na Ishmaeli (1-16)

16  Basi Sarai, bibi ya Abramu hakukuwa amemuzalia watoto,+ lakini alikuwa na mutumishi Mumisri mwenye jina lake lilikuwa Hagari.+ 2  Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Tafazali unisikilize. Yehova amenizuia kuzaa watoto. Tafazali sasa, lala na mutumishi wangu. Pengine ninaweza kupata watoto kupitia yeye.”+ Kwa hiyo, Abramu akasikiliza mambo yenye Sarai alisema. 3  Kisha Abramu kuishi katika inchi ya Kanaani kwa miaka kumi (10), Sarai, bibi ya Abramu, akamuchukua Hagari, mutumishi wake Mumisri na kumupatia bwana yake Abramu akuwe bibi yake. 4  Kwa hiyo Abramu akalala na Hagari, na akapata mimba. Wakati alijua kwamba iko* na mimba, Hagari akaanza kumuzarau bimukubwa wake. 5  Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Ubaya wenye ninatendewa ni kosa lako. Ni mimi nilimutia mutumishi wangu katika mikono yako,* lakini wakati alijua kwamba iko* na mimba, akaanza kunizarau. Yehova ahukumu kati yangu na wewe.” 6  Kwa hiyo Abramu akamuambia Sarai: “Angalia! Mutumishi wako iko* chini ya mamlaka yako. Umutendee jambo lolote lenye unaona kuwa la muzuri.” Basi Sarai akaanza kumuonea, na Hagari akakimbia mbali naye. 7  Kisha wakati fulani malaika wa Yehova akamukuta Hagari kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi yenye ilikuwa katika njia ya kuenda Shuri.+ 8  Naye akasema: “Hagari, mutumishi wa Sarai, unatoka wapi na unaenda wapi?” Naye akajibu: “Ninakimbia mbali na bimukubwa wangu Sarai.” 9  Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Rudia kwa bimukubwa wako na ujinyenyekeze chini ya mukono wake.” 10  Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Nitafanya uzao wako ukuwe mwingi* sana, na kwa hiyo haitawezekana kuhesabia uzao huo kwa sababu ya wingi wake.”+ 11  Malaika wa Yehova akaongeza kusema: “Sasa uko na mimba, na utazaa mwana, na utamupatia jina Ishmaeli,* kwa maana Yehova ameona mateso yako. 12  Atakuwa kama punda wa pori.* Mukono wake utapigana na kila mutu; na mukono wa kila mutu utapigana naye, na atakaa akiwa mwenye kuangaliana na ndugu* zake wote.” 13  Kisha akaitia jina la Yehova, mwenye alikuwa anazungumuza naye: “Wewe ni Mungu mwenye kuona,”+ kwa maana alisema: “Je, kweli nimemuona yeye mwenye kuniona?” 14  Ndiyo sababu kisima hicho kiliitwa Beer-lahai-roi.* (Kiko kati ya Kadeshi na Beredi.) 15  Basi Hagari akamuzalia Abramu mwana, na Abramu akamupatia mwana wake, mwenye Hagari alizaa, jina Ishmaeli.+ 16  Abramu alikuwa na miaka makumi munane na sita (86) wakati Hagari alimuzaa Ishmaeli.

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Tnn., “katika kifua chako.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “mbegu yako ikuwe mingi.”
Maana yake “Mungu Anasikia.”
Ao “aina fulani ya punda wa pori,” hata kama watu fulani wanawaza kwamba ni pundamilia (zèbre). Inawezekana maneno hayo yanazungumuzia mutazamo wa kujitegemea.
Ao pengine “naye atakaa katika uadui na ndugu zake wote.”
Maana yake “Kisima cha Mwenye Kuishi Mwenye Ananiona.”