Mwanzo 4:1-26
4 Sasa Adamu akafanya ngono na Eva bibi yake, naye akapata mimba.+ Wakati alimuzaa Kaini,+ akasema: “Nimemuzaa* mutoto mwanaume kwa musaada wa Yehova.”
2 Kisha wakati fulani akazaa tena, Abeli+ ndugu yake.
Abeli akakuwa muchungaji wa kundi, lakini Kaini akakuwa mulimaji wa udongo.
3 Kisha wakati fulani, Kaini akaleta mazao ya shamba ili ayatolee Yehova.
4 Lakini Abeli alileta wazaliwa wa kwanza wa kundi lake,+ pamoja na mafuta ya wanyama hao. Hata kama Yehova alimukubali Abeli na toleo lake,+
5 hakumukubali Kaini na toleo lake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana na kuhuzunika.*
6 Kisha Yehova akamuambia Kaini: “Sababu gani unakasirika sana na kuhuzunika?
7 Ukibadilika na kutenda mambo ya muzuri, je, hautakubaliwa?* Lakini kama haubadilike na kutenda mambo ya muzuri, zambi inashutama kwenye mulango, na inatamani sana kukutawala; lakini je, utaishinda?”
8 Kisha mambo hayo Kaini akamuambia Abeli ndugu yake: “Tuende kwenye eneo la mashamba.” Basi wakati walikuwa kwenye eneo la mashamba, Kaini akamushambulia Abeli ndugu yake na akamuua.+
9 Kisha wakati fulani, Yehova akamuuliza Kaini: “Ndugu yako Abeli iko* wapi?” naye akajibu: “Sijue. Je, niko mulinzi wa ndugu yangu?”
10 Kwa hiyo Mungu akasema: “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako iko inanililia kutoka katika udongo.+
11 Na sasa umelaaniwa kwa kufukuzwa kutoka kwenye udongo wenye umefungua kinywa chake ili kupokea damu ya ndugu yako kutoka katika mukono wako.+
12 Wakati utalima udongo, hautakurudishia mazao yake.* Utakuwa mutu wa kutanga-tanga na mukimbizi katika dunia.”
13 Kwa hiyo Kaini akamuambia Yehova: “Azabu ya kosa langu ni kubwa sana, siwezi kuivumilia.
14 Leo unanifukuza kutoka katika inchi,* na mimi nitafichwa mbali na uso wako; na nitakuwa mutu wa kutanga-tanga na mukimbizi juu ya dunia, na kila mutu mwenye ataniona hakika ataniua.”
15 Kwa hiyo Yehova akamuambia: “Kwa sababu hiyo, mutu yeyote mwenye atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba (7).”
Basi Yehova akaweka alama kwa ajili ya Kaini ili kila mutu mwenye atamuona asimupige.
16 Kisha Kaini akatoka mbele ya Yehova na akaanza kuishi katika inchi ya Uhamisho,* upande wa mashariki wa Edeni.+
17 Kisha Kaini akafanya ngono na bibi yake,+ naye akapata mimba na kumuzaa Enoko. Kisha akajenga muji, akaita muji huo Enoko, jina la mwana wake.
18 Kisha wakati fulani Enoko akamuzaa Iradi. Na Iradi akamuzaa Mehuyaeli, na Mehuyaeli akamuzaa Metushaeli, na Metushaeli akamuzaa Lameki.
19 Lameki akachukua wanamuke wawili. Jina la mwanamuke wa kwanza lilikuwa Ada, na jina la wa pili lilikuwa Zila.
20 Ada akamuzaa Yabali. Alikuwa mwanzilishi wa wale wenye kuishi katika mahema na wenye kuwa na mifugo.
21 Jina la ndugu yake lilikuwa Yubali. Alikuwa mwanzilishi wa wale wote wenye kupiga kinubi na zumari.*
22 Pia, Zila alimuzaa Tubal-kaini, mwenye alitengeneza vyombo vya kila namna vya shaba na chuma. Na dada ya Tubal-kaini alikuwa Naama.
23 Kisha Lameki akatunga maneno haya kwa ajili ya bibi zake Ada na Zila:
“Musikie sauti yangu, ninyi bibi za Lameki;Musikilize maneno yangu:
Nimemuua mutu mumoja kwa sababu aliniumiza,Ndiyo, kijana mwanaume kwa sababu alinipiga.
24 Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba (7),+Basi Lameki ni mara makumi saba na saba (77).”
25 Adamu akafanya ngono tena na bibi yake, naye akamuzaa mwana. Akamuita jina Seti,*+ kwa sababu, alisema: “Mungu amenichagulia uzao mwingine* pa nafasi ya Abeli, kwa sababu Kaini alimuua.”+
26 Na Seti pia akamuzaa mwana, na akamuita jina Enoshi.+ Wakati huo watu wakaanza kuitia jina la Yehova.
Maelezo ya Chini
^ Ao “nimetokeza.”
^ Tnn., “uso wake ukaanguka.”
^ Ao “hautainuliwa?”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “nguvu zake.”
^ Tnn., “kutoka kwenye uso wa udongo.”
^ Ao “inchi ya Nodi.”
^ Ao “filimbi.”
^ Maana yake “Mwenye Amechaguliwa; Mwenye Amewekwa.”
^ Tnn., “mbegu ingine.”