Isaya 66:1-24

  • Ibada ya kweli na ibada ya uongo (1-6)

  • Mama Sayuni na wana wake (7-17)

  • Watu wanakusanyika Yerusalemu ili kuabudu (18-24)

66  Yehova anasema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha ufalme, na dunia ni kiti cha miguu yangu.+ Iko wapi, basi, nyumba yenye munaweza kunijengea,+Na mahali pangu pa kupumuzikia pako wapi?”+  2  “Mukono wangu mwenyewe umefanya vitu hivi vyote,Na vyote vilitokea hivi,” ni vile Yehova anasema.+ “Basi, nitamuangalia huyu,Mwenye kuwa munyenyekevu na mwenye kuvunjika katika roho na mwenye anatetemekea* neno langu.+  3  Mwenye anachinja ngombe-dume ni kama mwenye anapiga na kuua mwanadamu.+ Mwenye anachinja kondoo ni kama mwenye anavunja shingo ya imbwa.+ Mwenye anatoa zawadi⁠—kama damu ya nguruwe!+ Mwenye anatoa toleo la ubani la ukumbusho+ ni kama mwenye anabariki kwa maneno ya uchawi.*+ Wamechagua njia zao wenyewe,Na wanafurahia* mambo yenye kuchukiza.  4  Basi nitachagua njia za kuwapatia azabu,+Na nitaleta juu yao mambo yaleyale yenye wanaogopa. Kwa sababu wakati niliita, hakuna mwenye alijibu;Wakati nilisema, hakuna mwenye alisikiliza.+ Waliendelea kutenda mambo ya mubaya mbele ya macho yangu,Na walichagua kufanya mambo yenye kunichukiza.”+  5  Musikie neno la Yehova, ninyi wenye kutetemekea* neno lake: “Ndugu zenu wenye kuwachukia ninyi na kuwatenga kwa sababu ya jina langu, walisema, ‘Yehova atukuzwe!’+ Lakini Yeye atatokea na kuwaletea shangwe,Na ni wao ndio watapatishwa haya.”+  6  Kuko sauti ya makelele kutoka katika muji, sauti kutoka katika hekalu! Ni sauti ya Yehova akilipa maadui wake kile chenye wanastahili.  7  Mbele akuwe na uchungu wa kuzaa, alizaa.+ Mbele ashikwe na maumivu ya kuzaa, alizaa mutoto mwanaume.  8  Ni nani amekwisha kusikia jambo kama hilo? Ni nani ameona mambo kama hayo? Je, inchi itazaliwa katika siku moja? Ao, je, taifa lote litazaliwa mara moja? Lakini, wakati tu Sayuni alikuwa na uchungu wa kuzaa, alizaa wana wake.  9  “Je, nitafanya akaribie kuzaliwa na kisha nifanye asizaliwe?” ni vile Yehova anasema. “Ao, je, nitatokeza kuzaliwa na kisha nifunge tumbo la uzazi?” ni vile Mungu wako anasema. 10  Mushangilie pamoja na Yerusalemu na mufurahi pamoja naye,+ ninyi wote wenye kumupenda.+ Mufurahi sana pamoja naye, ninyi wote wenye kumuombolezea, 11  Kwa maana mutanyonya na kushiba kabisa kutokana na maziwa yake ya faraja,Na mutakunywa sana na kupata furaha katika utukufu wake mwingi. 12  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Angalia, ninamupatia amani kama vile muto+Na utukufu wa mataifa kama muto wenye kufurika.+ Mutanyonya na kubebwa kwenye kiuno,Na mutachezeshwa kwenye magoti. 13  Kama vile mama anamufariji mwana wake,Ni vile nitaendelea kuwafariji;+Na mutafarijiwa kuhusiana na Yerusalemu.+ 14  Mutaona jambo hilo, na moyo wenu utashangilia,Mifupa yenu itasitawi kama vile majani ya mupya. Na mukono wa Yehova utajulikana* kwa watumishi wake,Lakini atalaumu maadui wake.”+ 15  “Kwa maana Yehova atakuja kama moto,+Na magari yake yako kama upepo wa zoruba,+Ili kulipa kwa kasirani kali,Ili kukemea kwa miali ya moto.+ 16  Kwa maana Yehova ataleta hukumu kwa moto,Ndiyo, kwa upanga wake, juu ya miili yote;*Na wenye watauawa na Yehova watakuwa wengi. 17  “Wale wenye kujitakasa na kujisafisha ili waingie kwenye mabustani*+ wakimufuata ule mwenye kuwa katikati, wale wenye kula nyama ya nguruwe+ na vitu vyenye kuchukiza na panya,+ wote watafikia mwisho wao pamoja,” ni vile Yehova anasema. 18  “Kwa kuwa ninajua kazi zao na mawazo yao, ninakuja kukusanya watu wa mataifa yote na luga zote, na watakuja na kuona utukufu wangu.” 19  “Nitatia alama kati yao, na wamoja kati ya wale wenye waliponyoka, nitawatuma kwenye mataifa haya: Tarshishi,+ Pulu, na Ludi,+ wale wenye wanakokota upinde, Tubali na Yavani,+ na visiwa vya mbali sana⁠—​wenye hawajasikia habari juu yangu wala kuona utukufu wangu; na watatangaza utukufu wangu kati ya mataifa.+ 20  Wataleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ ili wakuwe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari, ndani ya magari ya kukokotwa yenye kufunikwa, juu ya nyumbu, na juu ya ngamia wenye kuenda haraka, mupaka kwenye mulima wangu mutakatifu, Yerusalemu,” ni vile Yehova anasema, “kama vile watu wa Israeli wanaleta ndani ya nyumba ya Yehova zawadi yao katika chombo safi.” 21  “Pia nitakamata wamoja kwa ajili ya makuhani na kwa ajili ya Walawi,” ni vile Yehova anasema. 22  “Kwa maana kama vile mbingu mupya na dunia mupya+ vyenye ninafanya vitaendelea kusimama mbele yangu,” ni vile Yehova anasema, “vilevile uzao wenu* na jina lenu vitaendelea.”+ 23  “Na kutoka mwezi mupya mupaka mwezi mupya na kutoka sabato mupaka sabato,Miili yote itaingia* ili kuinama mbele yangu,”*+ ni vile Yehova anasema. 24  “Na wataenda na kuangalia mizoga ya wale wenye waliniasi;Kwa maana minyoo yenye kuwa juu yao haitakufa,Na moto wao hautazimika,+Na watakuwa chukizo kwa watu wote.”*

Maelezo ya Chini

Ao “mwenye kuhangaikia.”
Ao pengine, “mwenye anasifu sanamu.”
Ao “nafsi yao inafurahia.”
Ao “wenye kuhangaikia.”
Ao “nguvu za Yehova zitajulikana.”
Ao “wanadamu wote.”
Ni kusema, mabustani ya pekee yenye yalitumiwa kwa ajili ya ibada ya sanamu.
Tnn., “mbegu yenu.”
Ao “wanadamu wote.”
Ao “kuniabudu.”
Tnn., “wote wenye mwili.”