Isaya 30:1-33

  • Musaada wa Misri hauna mafaa yoyote kabisa (1-7)

  • Watu wanakataa ujumbe wa unabii (8-14)

  • Mutakuwa na nguvu kama munakuwa na tumaini (15-17)

  • Yehova anaonyesha watu wake wema (18-26)

    • Yehova, Mufundishaji Mukubwa (20)

    • “Hii ndiyo njia” (21)

  • Yehova ataleta hukumu juu ya Ashuru (27-33)

30  “Ole wao wana wenye wako kichwa-nguvu,”+ ni vile Yehova anasema,“Wenye wanatimiza mipango yenye haiko yangu,+Wenye wanafanya maagano,* lakini haiko kwa roho yangu,Ili kuongeza zambi juu ya zambi.  2  Wanashuka kuenda Misri+ bila kuniuliza,*+Ili kujiweka chini ya ulinzi wa Farao*Na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!  3  Lakini ulinzi wa Farao utawaletea ninyi haya,Na kimbilio katika kivuli cha Misri litafanya mufezeheke.+  4  Kwa maana wakubwa wake wako Soani,+Na wajumbe wake wamefika Hanesi.  5  Wote watapatishwa hayaNa watu wenye hawawezi kuwaletea faida,Wenye hawatoe musaada wala faida,Isipokuwa tu haya na aibu.”+ 6  Tangazo juu ya wanyama wa kusini: Katika inchi ya taabu na hali ngumu,Ya simba, simba mwenye kunguruma,Ya nyoka-kipiri na nyoka wa moto mwenye kuruka,*Wanabeba mali zao juu ya migongo ya pundaNa mizigo yao juu ya sehemu zenye kuvimba za migongo ya ngamia. Lakini vitu hivyo havitaletea watu faida.  7  Kwa maana musaada wa Misri hauna mafaa yoyote.+ Kwa hiyo nimemuita huyu: “Rahabu,+ mwenye kukaa bila kutikisika.”  8  “Sasa uende, uiandike juu ya bamba mbele yao,Na uiandike katika kitabu,+Ili itumike siku yenye kujaKama ushahidi wa kudumu.+  9  Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wadanganyifu,+Wana wenye hawataki kusikia sheria ya* Yehova.+ 10  Wanaambia waonaji, ‘Musione,’Na wale wenye kupata maono, ‘Musituambie maono ya kweli.+ Mutuambie mambo ya kusifu-sifu;* muone maono ya udanganyifu.+ 11  Mutoke katika njia; muondoke katika pito. Muache kutia Mutakatifu wa Israeli mbele yetu.’”+ 12  Kwa hiyo Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: “Kwa sababu munakataa neno hili,+Na munategemea upunjaji na udanganyifuNa munategemea mambo hayo,+ 13  Kwa hiyo kosa hili litakuwa kwenu kama ukuta wenye kubomoka,Kama ukuta murefu wenye kuvimba wenye unakaribia kuanguka,Utaanguka kwa kushitukia, mara moja. 14  Utavunjwa kama vile mutungi mukubwa wa mufinyanzi,*Utapondwa kabisa na hivyo hakuna kipande kati ya vipande vyake chenye kitabakiaIli kutumiwa kukusanya moto katika jikoAo kushota maji kwenye kiziwa cha maji.”* 15  Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: “Kama munanirudilia na kupumuzika, mutaokolewa;Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”+ Lakini hamukutaka.+ 16  Lakini, mulisema: “Hapana, tutakimbia kwa farasi!” Basi mutakimbia. “Na tutapanda farasi wenye kuenda mbio!”+ Kwa hiyo wale wenye kuwafuatilia watakuwa na mbio.+ 17  Watu elfu moja (1 000) watatetemeka kwa kuogopeshwa na mutu mumoja;+Wakati mutaogopeshwa na watu tano (5) mutakimbiaMupaka wakati watu wenye watabakia kati yenu watakuwa kama mulingoti kwenye kichwa cha mulimaKama nguzo ya alama juu ya kilima.+ 18  Lakini Yehova anawangojea kwa uvumilivu* ili awaonyeshe wema,+Na atasimama ili kuwaonyesha rehema.+ Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki.+ Wenye furaha ni wale wote wenye wanaendelea kumungojea.*+ 19  Wakati watu watakaa katika Sayuni, katika Yerusalemu,+ hautalia tena.+ Hakika atakuonyesha wema wakati utalia kwa sauti kubwa ili kuomba musaada; atakujibu wakati tu atasikia kilio chako.+ 20  Hata kama Yehova atawapatia ninyi mukate kwa namna ya taabu na maji kwa namna ya ukandamizaji,+ Mufundishaji wako Mukubwa hatajificha tena, na utamuona Mufundishaji wako Mukubwa+ kwa macho yako mwenyewe. 21  Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako likisema, “Hii ndiyo njia.+ Mutembee ndani yake,” ikuwe mutaenda upande wa kuume ao mutaenda upande wa kushoto.+ 22  Na mutachafua feza yenye inafunika sanamu zenu za kuchongwa na zahabu yenye inafunika sanamu zenu za metali.*+ Mutazitupa kama kipande cha nguo chenye mwanamuke anatumia katika siku zake za kuona mwezi* na kuziambia: “Mupotelee mbali!”*+ 23  Na ataleta mvua kwa ajili ya mbegu zenye utapanda katika udongo,+ na mukate wenye udongo utatokeza utakuwa mwingi na wenye kujenga mwili.*+ Siku hiyo mifugo yako itakula majani katika malisho yenye nafasi kubwa.+ 24  Na ngombe na punda wenye kulima udongo watakula chakula chenye kukolezwa kwa majani yenye uchachu, chenye kupepuliwa kwa kipao* na kwa kanya.* 25  Na juu ya kila mulima murefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuwa mito midogo-midogo na mifereji ya maji,+ katika siku ya mauaji makubwa wakati minara itaanguka. 26  Na mwangaza wa mwezi wenye kuenea utakuwa kama mwangaza wa jua; na mwangaza wa jua utaongezeka mara saba (7),+ kama mwangaza wa siku saba, katika siku yenye Yehova atafunga kuvunjika kwa watu wake+ na kuponyesha kidonda kikubwa chenye kilitokana na pigo lenye alileta.+ 27  Angalia! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali,Likiwaka kwa hasira yake na kwa mawingu mazito. Na midomo yake imejaa kasirani kali,Na ulimi wake ni kama moto wenye kuteketeza.+ 28  Roho* yake ni kama muto wenye kujaa sana wenye unafika mupaka kwenye shingo,Ili kutikisa mataifa katika chombo cha kuchujia cha uharibifu;*Na vikundi vya watu vitakuwa na lijamu*+ yenye kuwapotosha katika mataya* yao. 29  Lakini wimbo wenu utakuwa kama wimbo wenye kuimbwa usikuWakati munajitayarisha* kwa ajili ya sikukuu,+Na moyo wenu utafurahi sana kama mutuMwenye anatembea na* filimbiAkielekea kwenye mulima wa Yehova, kwa Mwamba wa Israeli.+ 30  Yehova atafanya sauti yake kubwa+ isikikeNa ataonyesha mukono wake+ wakati unashuka kwa kasirani kali,+Ukiwa na mwali wa moto wenye kuteketeza,+Mvua nyingi ya kushitukia+ na zoruba yenye mungurumo na mvua ya majiwe.+ 31  Kwa sababu ya sauti ya Yehova, Ashuru itashikwa na woga mukubwa;+Yeye ataipiga kwa fimbo.+ 32  Na kila pigo la fimbo yake ya azabuLenye Yehova ataleta juu ya AshuruLitasindikizwa na ngoma za kidogo* na vinubi;+Wakati anatikisa mukono wake juu yao katika vita.+ 33  Kwa maana Tofeti* yake+ tayari imetayarishwa;Pia imetayarishwa kwa ajili ya mufalme.+ Amefanya rundo lake la kuni likuwe na urefu kuenda chini na upana,Kwa wingi wa moto na kuni. Pumuzi ya Yehova, kama muto wa kiberiti,Itaiwasha moto.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Wenye wanamwanga sadaka ya kinywaji,” inaonekana ni kufanya makubaliano.
Tnn., “katika ngome ya Farao.”
Ao “bila kuuliza kinywa changu.”
Ao “nyoka mwenye sumu mwenye anaruka-ruka.”
Ao “agizo la.”
Tnn., “laini.”
Ao pengine, “tangi.”
Ao “wenye wanamungojea kwa hamu.”
Ao “anaendelea kuwangojea.”
Ao “sanamu za kuyeyushwa.”
Ao “hezi.”
Ao pengine, “na kuziita uchafu.”
Tnn., “munene na wenye mafuta.”
Ao “sepetu; bêche.”
Ao “uma.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
Tnn., “kichujio chenye hakina mafaa yoyote.”
Ao “Pumuzi.”
Ao “munajitakasa.”
Ao “kwa sauti ya.”
Ao “matari.”
Hapa neno “Tofeti” linatumiwa kama mahali pa mufano pa kuchomea vitu, linafananisha uharibifu.