Isaya 30:1-33
30 “Ole wao wana wenye wako kichwa-nguvu,”+ ni vile Yehova anasema,“Wenye wanatimiza mipango yenye haiko yangu,+Wenye wanafanya maagano,* lakini haiko kwa roho yangu,Ili kuongeza zambi juu ya zambi.
2 Wanashuka kuenda Misri+ bila kuniuliza,*+Ili kujiweka chini ya ulinzi wa Farao*Na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!
3 Lakini ulinzi wa Farao utawaletea ninyi haya,Na kimbilio katika kivuli cha Misri litafanya mufezeheke.+
4 Kwa maana wakubwa wake wako Soani,+Na wajumbe wake wamefika Hanesi.
5 Wote watapatishwa hayaNa watu wenye hawawezi kuwaletea faida,Wenye hawatoe musaada wala faida,Isipokuwa tu haya na aibu.”+
6 Tangazo juu ya wanyama wa kusini:
Katika inchi ya taabu na hali ngumu,Ya simba, simba mwenye kunguruma,Ya nyoka-kipiri na nyoka wa moto mwenye kuruka,*Wanabeba mali zao juu ya migongo ya pundaNa mizigo yao juu ya sehemu zenye kuvimba za migongo ya ngamia.
Lakini vitu hivyo havitaletea watu faida.
7 Kwa maana musaada wa Misri hauna mafaa yoyote.+
Kwa hiyo nimemuita huyu: “Rahabu,+ mwenye kukaa bila kutikisika.”
8 “Sasa uende, uiandike juu ya bamba mbele yao,Na uiandike katika kitabu,+Ili itumike siku yenye kujaKama ushahidi wa kudumu.+
9 Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wadanganyifu,+Wana wenye hawataki kusikia sheria ya* Yehova.+
10 Wanaambia waonaji, ‘Musione,’Na wale wenye kupata maono, ‘Musituambie maono ya kweli.+
Mutuambie mambo ya kusifu-sifu;* muone maono ya udanganyifu.+
11 Mutoke katika njia; muondoke katika pito.
Muache kutia Mutakatifu wa Israeli mbele yetu.’”+
12 Kwa hiyo Mutakatifu wa Israeli anasema hivi:
“Kwa sababu munakataa neno hili,+Na munategemea upunjaji na udanganyifuNa munategemea mambo hayo,+
13 Kwa hiyo kosa hili litakuwa kwenu kama ukuta wenye kubomoka,Kama ukuta murefu wenye kuvimba wenye unakaribia kuanguka,Utaanguka kwa kushitukia, mara moja.
14 Utavunjwa kama vile mutungi mukubwa wa mufinyanzi,*Utapondwa kabisa na hivyo hakuna kipande kati ya vipande vyake chenye kitabakiaIli kutumiwa kukusanya moto katika jikoAo kushota maji kwenye kiziwa cha maji.”*
15 Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi:
“Kama munanirudilia na kupumuzika, mutaokolewa;Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”+
Lakini hamukutaka.+
16 Lakini, mulisema: “Hapana, tutakimbia kwa farasi!”
Basi mutakimbia.
“Na tutapanda farasi wenye kuenda mbio!”+
Kwa hiyo wale wenye kuwafuatilia watakuwa na mbio.+
17 Watu elfu moja (1 000) watatetemeka kwa kuogopeshwa na mutu mumoja;+Wakati mutaogopeshwa na watu tano (5) mutakimbiaMupaka wakati watu wenye watabakia kati yenu watakuwa kama mulingoti kwenye kichwa cha mulimaKama nguzo ya alama juu ya kilima.+
18 Lakini Yehova anawangojea kwa uvumilivu* ili awaonyeshe wema,+Na atasimama ili kuwaonyesha rehema.+
Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki.+
Wenye furaha ni wale wote wenye wanaendelea kumungojea.*+
19 Wakati watu watakaa katika Sayuni, katika Yerusalemu,+ hautalia tena.+ Hakika atakuonyesha wema wakati utalia kwa sauti kubwa ili kuomba musaada; atakujibu wakati tu atasikia kilio chako.+
20 Hata kama Yehova atawapatia ninyi mukate kwa namna ya taabu na maji kwa namna ya ukandamizaji,+ Mufundishaji wako Mukubwa hatajificha tena, na utamuona Mufundishaji wako Mukubwa+ kwa macho yako mwenyewe.
21 Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako likisema, “Hii ndiyo njia.+ Mutembee ndani yake,” ikuwe mutaenda upande wa kuume ao mutaenda upande wa kushoto.+
22 Na mutachafua feza yenye inafunika sanamu zenu za kuchongwa na zahabu yenye inafunika sanamu zenu za metali.*+ Mutazitupa kama kipande cha nguo chenye mwanamuke anatumia katika siku zake za kuona mwezi* na kuziambia: “Mupotelee mbali!”*+
23 Na ataleta mvua kwa ajili ya mbegu zenye utapanda katika udongo,+ na mukate wenye udongo utatokeza utakuwa mwingi na wenye kujenga mwili.*+ Siku hiyo mifugo yako itakula majani katika malisho yenye nafasi kubwa.+
24 Na ngombe na punda wenye kulima udongo watakula chakula chenye kukolezwa kwa majani yenye uchachu, chenye kupepuliwa kwa kipao* na kwa kanya.*
25 Na juu ya kila mulima murefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuwa mito midogo-midogo na mifereji ya maji,+ katika siku ya mauaji makubwa wakati minara itaanguka.
26 Na mwangaza wa mwezi wenye kuenea utakuwa kama mwangaza wa jua; na mwangaza wa jua utaongezeka mara saba (7),+ kama mwangaza wa siku saba, katika siku yenye Yehova atafunga kuvunjika kwa watu wake+ na kuponyesha kidonda kikubwa chenye kilitokana na pigo lenye alileta.+
27 Angalia! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali,Likiwaka kwa hasira yake na kwa mawingu mazito.
Na midomo yake imejaa kasirani kali,Na ulimi wake ni kama moto wenye kuteketeza.+
28 Roho* yake ni kama muto wenye kujaa sana wenye unafika mupaka kwenye shingo,Ili kutikisa mataifa katika chombo cha kuchujia cha uharibifu;*Na vikundi vya watu vitakuwa na lijamu*+ yenye kuwapotosha katika mataya* yao.
29 Lakini wimbo wenu utakuwa kama wimbo wenye kuimbwa usikuWakati munajitayarisha* kwa ajili ya sikukuu,+Na moyo wenu utafurahi sana kama mutuMwenye anatembea na* filimbiAkielekea kwenye mulima wa Yehova, kwa Mwamba wa Israeli.+
30 Yehova atafanya sauti yake kubwa+ isikikeNa ataonyesha mukono wake+ wakati unashuka kwa kasirani kali,+Ukiwa na mwali wa moto wenye kuteketeza,+Mvua nyingi ya kushitukia+ na zoruba yenye mungurumo na mvua ya majiwe.+
31 Kwa sababu ya sauti ya Yehova, Ashuru itashikwa na woga mukubwa;+Yeye ataipiga kwa fimbo.+
32 Na kila pigo la fimbo yake ya azabuLenye Yehova ataleta juu ya AshuruLitasindikizwa na ngoma za kidogo* na vinubi;+Wakati anatikisa mukono wake juu yao katika vita.+
33 Kwa maana Tofeti* yake+ tayari imetayarishwa;Pia imetayarishwa kwa ajili ya mufalme.+
Amefanya rundo lake la kuni likuwe na urefu kuenda chini na upana,Kwa wingi wa moto na kuni.
Pumuzi ya Yehova, kama muto wa kiberiti,Itaiwasha moto.
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Wenye wanamwanga sadaka ya kinywaji,” inaonekana ni kufanya makubaliano.
^ Tnn., “katika ngome ya Farao.”
^ Ao “bila kuuliza kinywa changu.”
^ Ao “nyoka mwenye sumu mwenye anaruka-ruka.”
^ Ao “agizo la.”
^ Tnn., “laini.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao pengine, “tangi.”
^ Ao “wenye wanamungojea kwa hamu.”
^ Ao “anaendelea kuwangojea.”
^ Ao “sanamu za kuyeyushwa.”
^ Ao “hezi.”
^ Ao pengine, “na kuziita uchafu.”
^ Tnn., “munene na wenye mafuta.”
^ Ao “sepetu; bêche.”
^ Ao “uma.”
^ Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
^ Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
^ Tnn., “kichujio chenye hakina mafaa yoyote.”
^ Ao “Pumuzi.”
^ Ao “munajitakasa.”
^ Ao “kwa sauti ya.”
^ Ao “matari.”
^ Hapa neno “Tofeti” linatumiwa kama mahali pa mufano pa kuchomea vitu, linafananisha uharibifu.