Isaya 52:1-15
52 Amuka! Amuka! Uvae nguvu,+ Ee Sayuni!+
Vaa nguo zako zenye kupendeza,+ Ee Yerusalemu, muji mutakatifu!
Kwa maana mutu mwenye hatahiriwe na mutu mwenye haiko safi hawataingia ndani yako tena.+
2 Kunguta mavumbi, simama na ukae, Ee Yerusalemu.
Regeza minyororo yenye kuwa kwenye shingo yako, Ee binti ya Sayuni mwenye amekamatwa mateka.+
3 Kwa maana Yehova anasema hivi:
“Ninyi muliuzishwa bure,+Na mutakombolewa bila feza.”+
4 Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Pale mwanzo watu wangu waliteremuka kuenda Misri ili waishi kule wakiwa wageni;+Kisha Ashuru ikawakandamiza bila sababu.”
5 “Basi, nifanye nini hapa?” ni vile Yehova anasema.
“Kwa maana watu wangu walikamatwa bure.
Wale wenye kuwatawala wanaendelea kufanya makelele ya ushindi,”+ ni vile Yehova anasema,“Na kila wakati, muchana wote, jina langu linavunjiwa heshima.+
6 Kwa sababu hiyo watu wangu watajua jina langu;+Kwa sababu hiyo watajua siku hiyo kwamba mimi Ndiye ninasema.
Angalia! Ni mimi!”
7 Ni yenye kupendeza sana juu ya milima, miguu ya mutu mwenye kuleta habari njema,+Mwenye kutangaza amani,+Mwenye kuleta habari njema za jambo la muzuri zaidi,Mwenye kutangaza wokovu,Mwenye kuambia Sayuni: “Mungu wako amekuwa Mufalme!”+
8 Sikiliza! Walinzi wako wanapandisha sauti yao.
Wanapiga vigelegele vya shangwe pamoja,Kwa maana wataona jambo hilo waziwazi* wakati Yehova atakusanya tena Sayuni.
9 Muchangamuke, mupige pamoja vigelegele vya shangwe, ninyi mabomoko ya Yerusalemu,+Kwa maana Yehova amefariji watu wake;+ amekomboa Yerusalemu.+
10 Yehova ameonyesha waziwazi mukono wake mutakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+Miisho yote ya dunia itaona matendo ya wokovu ya* Mungu wetu.+
11 Mugeuke, mugeuke, mutoke kule,+ musiguse kitu chochote kichafu!+
Mutoke katikati yake,+ mujilinde mukiwa safi,Ninyi wenye kubeba vyombo vya Yehova.+
12 Kwa maana hamutaondoka mukiwa na woga mukubwa,Wala hamutahitaji kukimbia.Kwa maana Yehova ataenda mbele yenu,+Na Mungu wa Israeli atakuwa mulinzi wenu wa nyuma.+
13 Angalia! Mutumishi wangu+ atatenda kwa ufahamu.
Atainuliwa juu,Atainuliwa na kutukuzwa sana.+
14 Kama vile kulikuwa wengi wenye walimuangalia kwa mushangao—Kwa maana sura yake ilikuwa imeharibiwa kuliko ya mwanadamu yeyoteNa umbo yake ya heshima ilikuwa imeharibiwa kuliko ya wanadamu—
15 Basi atashitua mataifa mengi.+
Wafalme watafunga vinywa vyao* mbele yake,+Kwa sababu wataona mambo yenye hawakukuwa wameambiwa,Na kukazia uangalifu mambo yenye hawakukuwa wamesikia.+