Isaya 11:1-16

  • Utawala wenye haki wa tawi la Yese (1-10)

    • Imbwa wa pori na mwana-kondoo wanakaa pamoja (6)

    • Dunia itajaa ujuzi juu ya Yehova (9)

  • Mabaki wanarudishwa (11-16)

11  Na tawi+ litakomaa kutoka kwenye kisiki cha Yese,+Na chipukizi+ kutoka kwenye mizizi yake litazaa matunda.  2  Na roho ya Yehova itakaa juu yake,+Roho ya hekima+ na ya uelewaji,Roho ya shauri na ya nguvu,+Roho ya ujuzi na ya kumuogopa Yehova.  3  Na atapata shangwe katika kumuogopa Yehova.+ Hatahukumu kulingana na mambo yenye anaona kwa macho yake,Wala kukaripia kulingana tu na mambo yenye anasikia kwa masikio yake.+  4  Atahukumu kwa haki watu wa hali ya chini,Na kwa unyoofu atakaripia kwa ajili ya wapole wa dunia. Atapiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake+Na kuua waovu kwa pumuzi* ya midomo yake.+  5  Haki itakuwa mukaba* kwenye kifua chake,Na uaminifu mukaba wa viuno vyake.+  6  Imbwa wa pori atakaa pamoja na mwana-kondoo+ kwa wakati fulani,Na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi,Na kitoto-dume cha ngombe na simba* na munyama mwenye kunenepa wote watakuwa pamoja;*+Na kijana mudogo atawaongoza.  7  Ngombe na dubu watakula pamoja,Na vitoto vyao vitalala pamoja. Simba atakula majani kama ngombe-dume.+  8  Mutoto mwenye kunyonya atachezea juu ya shimo la nyoka-kobra,Na mutoto mwenye ameachishwa kunyonya atatia mukono wake juu ya tundu la nyoka mwenye sumu.  9  Hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza+Wala uharibifu wowote katika mulima wangu wote mutakatifu,+Kwa maana dunia hakika itajaa ujuzi juu ya YehovaKama vile maji yanafunika bahari.+ 10  Siku hiyo muzizi wa Yese+ utasimama kama alama* kwa ajili ya vikundi vya watu.+ Mataifa yatatafuta muongozo wake,*+Na mahali pake pa kupumuzikia patakuwa penye utukufu. 11  Siku hiyo Yehova atatoa tena mukono wake, mara ya pili, ili kurudisha mabaki ya watu wake wenye walibakia katika Ashuru,+ katika Misri,+ katika Patrosi,+ katika Kushi,+ katika Elamu,+ katika Shinari,* katika Hamati, na katika visiwa vya bahari.+ 12  Atasimamisha alama* kwa ajili ya mataifa na kukusanya watu wa Israeli wenye walisambazwa,+ na watu wa Yuda wenye walisambazwa atawakusanya pamoja kutoka pembe ine (4) za dunia.+ 13  Wivu wa Efraimu utaisha,+Na wale wenye kuonyesha Yuda uadui wataharibiwa. Efraimu hatasikilia Yuda wivu,Wala Yuda hataonyesha Efraimu uadui.+ 14  Nao watashuka kwenye miteremuko ya* Wafilisti upande wa mangaribi;Wakiwa pamoja watanyanganya vitu vya watu wa Mashariki. Watanyoosha mukono wao juu ya* Edomu+ na Moabu,+Na Waamoni watakuwa raia wao.+ 15  Yehova atagawanya* guba ya* bahari ya Misri,+Na kutikisa mukono wake juu ya ule Muto.*+ Kwa pumuzi* yake yenye kukausha ataipiga katika mito yake saba (7),*Na atafanya watu watembee na kuvuka wakiwa wamevaa viatu vyao. 16  Na kutakuwa njia kubwa+ kutoka Ashuru kwa ajili ya mabaki ya watu wake wenye watabakia,+Kama vile ilikuwa kwa ajili ya Israeli siku yenye alitoka katika inchi ya Misri.

Maelezo ya Chini

Ao “roho.”
Ao “mushipi.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao pengine, “Na kitoto-dume cha ngombe na simba watakula pamoja.”
Ao “Mataifa yatamutafuta.”
Ao “nguzo ya alama.”
Ni kusema, Babilonia.
Ao “nguzo ya alama.”
Tnn., “bega la.”
Ao “Watapanua mamlaka yao juu ya.”
Ao pengine, “atakausha.”
Tnn., “ulimi wa.” Guba ni sehemu ya bahari yenye inaingia katika inchi kavu.
Ni kusema, Efrati.
Ao “roho.”
Ao pengine, “ataipiga ikuwe mito 7.”