Isaya 11:1-16
11 Na tawi+ litakomaa kutoka kwenye kisiki cha Yese,+Na chipukizi+ kutoka kwenye mizizi yake litazaa matunda.
2 Na roho ya Yehova itakaa juu yake,+Roho ya hekima+ na ya uelewaji,Roho ya shauri na ya nguvu,+Roho ya ujuzi na ya kumuogopa Yehova.
3 Na atapata shangwe katika kumuogopa Yehova.+
Hatahukumu kulingana na mambo yenye anaona kwa macho yake,Wala kukaripia kulingana tu na mambo yenye anasikia kwa masikio yake.+
4 Atahukumu kwa haki watu wa hali ya chini,Na kwa unyoofu atakaripia kwa ajili ya wapole wa dunia.
Atapiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake+Na kuua waovu kwa pumuzi* ya midomo yake.+
5 Haki itakuwa mukaba* kwenye kifua chake,Na uaminifu mukaba wa viuno vyake.+
6 Imbwa wa pori atakaa pamoja na mwana-kondoo+ kwa wakati fulani,Na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi,Na kitoto-dume cha ngombe na simba* na munyama mwenye kunenepa wote watakuwa pamoja;*+Na kijana mudogo atawaongoza.
7 Ngombe na dubu watakula pamoja,Na vitoto vyao vitalala pamoja.
Simba atakula majani kama ngombe-dume.+
8 Mutoto mwenye kunyonya atachezea juu ya shimo la nyoka-kobra,Na mutoto mwenye ameachishwa kunyonya atatia mukono wake juu ya tundu la nyoka mwenye sumu.
9 Hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza+Wala uharibifu wowote katika mulima wangu wote mutakatifu,+Kwa maana dunia hakika itajaa ujuzi juu ya YehovaKama vile maji yanafunika bahari.+
10 Siku hiyo muzizi wa Yese+ utasimama kama alama* kwa ajili ya vikundi vya watu.+
Mataifa yatatafuta muongozo wake,*+Na mahali pake pa kupumuzikia patakuwa penye utukufu.
11 Siku hiyo Yehova atatoa tena mukono wake, mara ya pili, ili kurudisha mabaki ya watu wake wenye walibakia katika Ashuru,+ katika Misri,+ katika Patrosi,+ katika Kushi,+ katika Elamu,+ katika Shinari,* katika Hamati, na katika visiwa vya bahari.+
12 Atasimamisha alama* kwa ajili ya mataifa na kukusanya watu wa Israeli wenye walisambazwa,+ na watu wa Yuda wenye walisambazwa atawakusanya pamoja kutoka pembe ine (4) za dunia.+
13 Wivu wa Efraimu utaisha,+Na wale wenye kuonyesha Yuda uadui wataharibiwa.
Efraimu hatasikilia Yuda wivu,Wala Yuda hataonyesha Efraimu uadui.+
14 Nao watashuka kwenye miteremuko ya* Wafilisti upande wa mangaribi;Wakiwa pamoja watanyanganya vitu vya watu wa Mashariki.
Watanyoosha mukono wao juu ya* Edomu+ na Moabu,+Na Waamoni watakuwa raia wao.+
15 Yehova atagawanya* guba ya* bahari ya Misri,+Na kutikisa mukono wake juu ya ule Muto.*+
Kwa pumuzi* yake yenye kukausha ataipiga katika mito yake saba (7),*Na atafanya watu watembee na kuvuka wakiwa wamevaa viatu vyao.
16 Na kutakuwa njia kubwa+ kutoka Ashuru kwa ajili ya mabaki ya watu wake wenye watabakia,+Kama vile ilikuwa kwa ajili ya Israeli siku yenye alitoka katika inchi ya Misri.
Maelezo ya Chini
^ Ao “roho.”
^ Ao “mushipi.”
^ Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
^ Ao pengine, “Na kitoto-dume cha ngombe na simba watakula pamoja.”
^ Ao “Mataifa yatamutafuta.”
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Ni kusema, Babilonia.
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Tnn., “bega la.”
^ Ao “Watapanua mamlaka yao juu ya.”
^ Ao pengine, “atakausha.”
^ Tnn., “ulimi wa.” Guba ni sehemu ya bahari yenye inaingia katika inchi kavu.
^ Ni kusema, Efrati.
^ Ao “roho.”
^ Ao pengine, “ataipiga ikuwe mito 7.”