Isaya 20:1-6
-
Alama juu ya Misri na Etiopia (1-6)
20 Mwaka wenye Mufalme Sargoni wa Ashuru alituma Tartani* aende Ashdodi,+ alipigana na Ashdodi na akaikamata.+
2 Wakati huo Yehova alisema kupitia Isaya+ mwana wa Amozi, akisema: “Uende, utoshe nguo ya gunia kwenye viuno vyako; na utoshe viatu kwenye miguu yako.” Naye akafanya vile, akatembea huku na huku akiwa uchi* na miguu wazi.
3 Kisha Yehova akasema: “Kama vile Isaya mutumishi wangu alitembea huku na huku akiwa uchi na miguu wazi kwa miaka tatu (3) ili kuwa alama+ na jambo la ajabu juu ya Misri+ na juu ya Etiopia,+
4 vilevile mufalme wa Ashuru ataongoza watu wa Misri wenye walikamatwa mateka+ na wahamishwa wa Etiopia, vijana na wanaume wazee, wakiwa uchi na miguu wazi na matako wazi, uchi wa* Misri.
5 Na wataogopa sana na kupata haya kwa sababu ya Etiopia tumaini lao na kwa sababu ya Misri kiburi chao.*
6 Wakaaji wa inchi hii ya pembeni ya bahari watasema siku hiyo, ‘Angalia kile kilipata tumaini letu, lenye tulikimbilia ili kupata musaada na kukombolewa kutoka kwa mufalme wa Ashuru! Tutaponyoka namna gani sasa?’”
Maelezo ya Chini
^ Ao “kamanda.”
^ Ao “karibu uchi.”
^ Ao “haya ya.”
^ Ao “yenye wanavutiwa na uzuri wake.”