Isaya 39:1-8
-
Wajumbe kutoka Babiloni (1-8)
39 Wakati huo mufalme wa Babiloni, Merodak-baladani mwana wa Baladani, akamutumia Hezekia+ barua na zawadi, kwa maana alikuwa amesikia kwamba alikuwa mugonjwa na sasa amepona.+
2 Hezekia akawakaribisha kwa furaha* na kuwaonyesha nyumba yake ya hazina+—feza, zahabu, mafuta ya zeri na mafuta mengine yenye samani, depo yake yote ya silaha, na kila kitu chenye kilikuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chenye Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake mwenyewe* na katika eneo lote la utawala wake.
3 Kisha Isaya nabii akaingia kwa Mufalme Hezekia na kumuuliza: “Watu hawa walisema nini, na walitoka wapi?” Basi Hezekia akasema: “Walitoka katika inchi ya mbali, kule Babiloni.”+
4 Kisha akauliza: “Waliona nini katika nyumba yako?”* Hezekia akajibu: “Waliona kila kitu katika nyumba yangu.* Hakuna kitu chenye sikuwaonyesha katika hazina zangu.”
5 Sasa Isaya akamuambia Hezekia: “Sikia neno la Yehova wa majeshi,
6 ‘Angalia! Siku zinakuja, na vitu vyote vyenye kuwa katika nyumba yako* na vitu vyote vyenye mababu zako wameweka mupaka leo vitapelekwa Babiloni. Hakuna kitu chenye kitabakia,’+ ni vile Yehova anasema.+
7 ‘Na wamoja kati ya wana wako mwenyewe wenye utazaa watakamatwa na kuwa maofisa wa makao ya mufalme katika nyumba ya kifalme ya mufalme wa Babiloni.’”+
8 Halafu Hezekia akamuambia Isaya: “Neno la Yehova lenye umesema ni la muzuri.” Kisha akaongeza: “Kwa sababu kutakuwa amani na utulivu* wakati wa maisha yangu.”*+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “akashangilia kwa sababu yao.”
^ Ao “nyumba yake ya kifalme.”
^ Ao “nyumba yako ya kifalme?”
^ Ao “nyumba yangu ya kifalme.”
^ Ao “nyumba yako ya kifalme.”
^ Ao “kweli.”
^ Tnn., “siku zangu.”