Isaya 62:1-12

  • Jina mupya la Sayuni (1-12)

62  Sitanyamaza kwa ajili ya Sayuni,+Na sitatulia kwa ajili ya YerusalemuMupaka haki yake ingae kama mwangaza mukubwa,+Na wokovu wake uwake kama mwenge.+  2  “Mataifa yataona haki yako, Ee mwanamuke,+Na wafalme wote utukufu wako.+ Na utaitwa kwa jina mupya,+Lenye kinywa cha Yehova mwenyewe kitachagua.  3  Utakuwa taji la uzuri katika mukono wa Yehova,Kilemba cha kifalme katika mukono wa Mungu wako.  4  Hautaitwa tena mwanamuke mwenye aliachwa,+Na inchi yako haitaitwa tena yenye iliachwa ukiwa.+ Lakini utaitwa Ninapendezwa Naye,+Na inchi yako itaitwa Mwenye Kuolewa. Kwa maana Yehova atapendezwa na wewe,Na inchi yako itakuwa kama mwenye ameolewa.  5  Kwa maana kama vile kijana anaoa bikira,Ni vile wana wako watakuoa. Kama vile bwana-arusi anafurahia bibi-arusi,Ni vile Mungu wako atakufurahia.+  6  Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu. Kila wakati, muchana wote na usiku wote, hawapaswe kukaa kimya. Ninyi wenye kumutaja Yehova,Musipumuzike,  7  Na musiache apumuzike mupaka afanye Yerusalemu kuwa imara kabisa,Ndiyo, mupaka aifanye kuwa sifa ya dunia.”+  8  Yehova ameapa kwa mukono wake wa kuume, kwa mukono wake wenye nguvu: “Sitapatia tena maadui wako nafaka yako kuwa chakula,Wala wageni hawatakunywa divai yako mupya, yenye umefanyia kazi ya jasho.+  9  Lakini wale wenye kuikusanya wataikula na watamusifu Yehova;Na wale wenye kuikusanya wataikunywa katika viwanja vyangu vitakatifu.”+ 10  Mupite ndani yake, mupite katika milango mikubwa. Mutayarishie watu njia.+ Mutengeneze, mutengeneze njia kubwa. Muondoe majiwe ndani yake.+ Musimamishe alama* kwa ajili ya vikundi vya watu.+ 11  Angalia! Yehova ametangaza mupaka kwenye miisho ya dunia: “Muambie binti ya Sayuni,‘Angalia! Wokovu wako unakuja.+ Angalia! Zawabu yake iko pamoja naye,Na mushahara wenye analipa uko mbele yake.’”+ 12  Wataitwa watu watakatifu, wale wenye walikombolewa na Yehova,+Na utaitwa Mwenye Alitafutwa, Muji Wenye Haukuachwa.+

Maelezo ya Chini

Ao “nguzo ya alama.”