Isaya 5:1-30
5 Tafazali, acha nimuimbie mupendwa wanguWimbo kuhusu mupenzi wangu na shamba lake la mizabibu.+
Mupendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye kuzaa sana.
2 Alililima na kuondoa majiwe ndani yake.
Alipanda muzabibu muzuri mwekundu,Alijenga munara katikati yake,Na alichimba kikamulio cha divai ndani yake.+
Kisha akaendelea kutumaini lizae zabibu,Lakini lilizaa tu zabibu za pori.+
3 “Na sasa, ninyi wakaaji wa Yerusalemu na watu wa Yuda,Tafazali muhukumu kati yangu na shamba langu la mizabibu.+
4 Ni jambo gani lingine lenye ningefanyia shamba langu la mizabibuLenye sijafanya?+
Sababu gani, wakati nilitumaini lizae zabibu,Lilizaa tu zabibu za pori?
5 Sasa, tafazali, acha niwaambieKile nitafanyia shamba langu la mizabibu:
Nitaondoa lupango yake,Na litateketezwa kwa moto.+
Nitabomoa ukuta wake wa majiwe,Na litakanyangwa-kanyangwa.
6 Na nitalifanya kuwa eneo lenye limeachwa;+Halitapunguzwa matawi wala kulimwa.
Nalo litaota miti midogo-midogo ya miiba na magugu,+Na nitaamuru mawingu yasitume mvua yoyote juu yake.+
7 Kwa maana shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli;+Watu wa Yuda ndilo shamba lenye alikuwa anapenda sana.
Aliendelea kutumaini haki,+Lakini angalia! kulikuwa ukosefu wa haki;Alitumaini uadilifu,*Lakini angalia! kulikuwa kilio cha uchungu.”+
8 Ole wao wale wenye wanaunganisha nyumba moja na nyumba ingine,+Na wenye wanaunganisha shamba moja na shamba lingine+Mupaka hakuna tena nafasiNa ninyi munaishi peke yenu katika inchi!
9 Yehova wa majeshi ameapa katika masikio yanguKwamba nyumba nyingi, hata kama ziko kubwa na za muzuri,Zitakuwa kitu cha kuogopesha sana,Bila mukaaji.+
10 Kwa maana ekari kumi (10)* za shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bati,*Na kipimo kimoja cha homeri* ya mbegu kitazaa efa* moja tu.+
11 Ole wao wale wenye wanaamuka asubui sana ili wakunywe pombe,+Wenye wanakawia mupaka giza la mangaribi sana kufikia wakati divai inawaka kama moto ndani yao!
12 Wako na kinubi na chombo cha kamba,Ngoma ya kidogo,* filimbi, na divai kwenye karamu zao;Lakini hawafikirie kazi za Yehova,Wala hawaone kazi ya mikono yake.
13 Kwa hiyo watu wangu wataenda katika uhamishoKwa sababu ya kukosa ujuzi;+Watu wao wenye utukufu watakuwa na njaa,+Na watu wao wote watakauka kwa kiu.
14 Kwa hiyo Kaburi* limejipanua*Na limefungua kinywa chake bila mwisho;+Na utukufu wake,* vikundi vyake vya watu wenye makelele, na watu wake wenye kushangiliaHakika watashuka ndani yake.
15 Na mwanadamu atainama,Mwanadamu atashushwa,Na macho ya wenye majivuno yatashushwa.
16 Yehova wa majeshi atainuliwa kupitia hukumu* yake;Mungu wa kweli, Mutakatifu,+ atajitakasa kupitia haki.+
17 Na wana-kondoo watakula majani kama katika malisho yao;Wakaaji wageni watakula katika maeneo yenye ukiwa ya wanyama wenye kukulishwa muzuri.
18 Ole wao wale wenye wanakokota hatia yao kwa kamba za udanganyifuNa zambi yao kwa kamba za gari la kukokotwa;
19 Wale wenye kusema: “Acha Yeye afanye haraka kazi yake;Acha ikuje haraka ili tuione.
Acha kusudi la* Mutakatifu wa Israeli litendekeIli tulijue!”+
20 Ole wao wale wenye kusema kwamba wema ni ubaya na ubaya ni wema,+Wale wenye kutia giza pa nafasi ya mwangaza na mwangaza pa nafasi ya giza,Wale wenye kutia uchungu pa nafasi ya utamu na utamu pa nafasi ya uchungu!
21 Ole wao wale wenye hekima mbele ya macho yao wenyewe,Na wenye busara mbele ya macho yao wenyewe!+
22 Ole wao wale wenye wako na nguvu katika kunywa divai,Na wanaume wenye wako mafundi wa kuchanganya pombe,+
23 Wale wenye wanamuondolea muovu hatia kwa rushwa,*+Na wenye wanamuima haki mwenye haki!+
24 Kwa hiyo, kama vile mwali wa moto unateketeza majani ya kukaukaNa kama vile majani ya kukauka yanajikunja katika miali ya moto,Mizizi yao itaoza,Na maua yao yatasambaa kama unga,Kwa sababu walikataa sheria ya* Yehova wa majeshi,Na walizarau neno la Mutakatifu wa Israeli.+
25 Ndiyo sababu kasirani ya Yehova inawaka juu ya watu wake,Na atanyoosha mukono wake juu yao na kuwapiga.+
Milima itatetemeka,Na maiti zao zitakuwa kama uchafu katika barabara.+
Kwa sababu ya mambo hayo yote, kasirani yake haijarudia nyuma,Lakini mukono wake ungali wenye kunyooshwa ili kupiga.
26 Amesimamishia alama* taifa la mbali;+Amewapigia muluzi ili wakuje kutoka miisho ya dunia;+Na angalia! wanakuja mbio sana.+
27 Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye kuchoka wala kujikwaa.
Hakuna mwenye kusinzia wala kulala.
Mukaba* wenye kuwa kwenye kiuno chao haujaregezwa,Wala kamba za viatu vyao hazijakatika.
28 Mishale yao yote ni mikali,Na pinde zao zote zimekunjwa.*
Kwato* za farasi zao ziko kama jiwe ngumu,Na magurudumu* yao kama upepo wa zoruba.+
29 Mungurumo wao ni kama wa simba;Wananguruma kama wana-simba.*+
Watanguruma na kukamata mawindoNa kubeba mawindo hayo bila mutu wa kuyakomboa.
30 Siku hiyo watanguruma juu yakeKama mungurumo wa bahari.+
Mutu yeyote mwenye kuangalia inchi ataona giza lenye kuogopesha;Hata mwangaza umetiwa giza kwa sababu ya mawingu.+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “shubiri 10.”
^ Angalia Nyongeza B14.
^ Angalia Nyongeza B14.
^ Angalia Nyongeza B14.
^ Ao “tari.”
^ Ao “watu wake wenye vyeo.”
^ Ao “limepanua nafsi yake.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “haki.”
^ Ao “uamuzi wa; shauri la.”
^ Ao “kata-midomo.”
^ Ao “agizo la.”
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Ao “Mushipi.”
^ Ao “ziko tayari kutupa mishale.”
^ Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
^ Ao “mipeto; pneus.”
^ Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”