Isaya 15:1-9

  • Tangazo juu ya Moabu (1-9)

15  Tangazo juu ya Moabu:+ Kwa sababu imeharibiwa katika usiku mumoja,Ari+ ya Moabu imenyamazishwa. Kwa sababu imeharibiwa katika usiku mumoja,Kiri+ ya Moabu imenyamazishwa.  2  Ameenda mupaka kwenye Nyumba* na mupaka Diboni,+Kwenye mahali pa juu ili kulia. Moabu inaombolezea Nebo+ na Medeba.+ Kila kichwa kimenyolewa upara,+ ndevu zote zimenyolewa.+  3  Wamevaa nguo za magunia katika barabara zake. Kwenye sehemu za juu za nyumba zao na katika viwanja vya watu wote, wote wanaomboleza;Wanashuka wakilia.+  4  Heshboni na Eleale+ wanalia;Sauti yao inasikika mupaka Yahazi.+ Ndiyo sababu watu wenye kubeba silaha wa Moabu wanaendelea kupandisha sauti. Anatetemeka.*  5  Moyo wangu unamulilia Moabu. Wakimbizi wake wamekimbia mupaka Soari+ na Eglat-shelishiya.+ Kwenye mupando wa Luhiti wanalia wakipanda;Kwenye njia ya kuenda Horonaimu wanalia kwa sauti kubwa kwa sababu ya musiba.+  6  Kwa maana maji ya Nimrimu yameachwa bila kitu;Majani ya mubichi yamekauka,Majani yameisha na hakuna kitu chochote cha mubichi chenye kimebakia.  7  Ndiyo sababu wanabeba kile kilibakia katika madepo yao na utajiri wao;Wanavuka bonde* la miti ya mierebi.  8  Kwa maana kilio kinasikika katika eneo lote la Moabu.+ Maombolezo yanafika Eglaimu;Maombolezo yanafika Beer-elimu.  9  Kwa maana maji ya Dimoni yamejaa damu. Na niko na mengi zaidi kwa ajili ya Dimoni: Simba kwa ajili ya wale wa Moabu wenye wanaponyokaNa kwa ajili ya wale wenye kubakia katika inchi.+

Maelezo ya Chini

Ao “Hekalu.”
Ao “Nafsi yake inatetemeka.”
Ao “bonde la muto.”