Isaya 15:1-9
-
Tangazo juu ya Moabu (1-9)
15 Tangazo juu ya Moabu:+
Kwa sababu imeharibiwa katika usiku mumoja,Ari+ ya Moabu imenyamazishwa.
Kwa sababu imeharibiwa katika usiku mumoja,Kiri+ ya Moabu imenyamazishwa.
2 Ameenda mupaka kwenye Nyumba* na mupaka Diboni,+Kwenye mahali pa juu ili kulia.
Moabu inaombolezea Nebo+ na Medeba.+
Kila kichwa kimenyolewa upara,+ ndevu zote zimenyolewa.+
3 Wamevaa nguo za magunia katika barabara zake.
Kwenye sehemu za juu za nyumba zao na katika viwanja vya watu wote, wote wanaomboleza;Wanashuka wakilia.+
4 Heshboni na Eleale+ wanalia;Sauti yao inasikika mupaka Yahazi.+
Ndiyo sababu watu wenye kubeba silaha wa Moabu wanaendelea kupandisha sauti.
Anatetemeka.*
5 Moyo wangu unamulilia Moabu.
Wakimbizi wake wamekimbia mupaka Soari+ na Eglat-shelishiya.+
Kwenye mupando wa Luhiti wanalia wakipanda;Kwenye njia ya kuenda Horonaimu wanalia kwa sauti kubwa kwa sababu ya musiba.+
6 Kwa maana maji ya Nimrimu yameachwa bila kitu;Majani ya mubichi yamekauka,Majani yameisha na hakuna kitu chochote cha mubichi chenye kimebakia.
7 Ndiyo sababu wanabeba kile kilibakia katika madepo yao na utajiri wao;Wanavuka bonde* la miti ya mierebi.
8 Kwa maana kilio kinasikika katika eneo lote la Moabu.+
Maombolezo yanafika Eglaimu;Maombolezo yanafika Beer-elimu.
9 Kwa maana maji ya Dimoni yamejaa damu.Na niko na mengi zaidi kwa ajili ya Dimoni:
Simba kwa ajili ya wale wa Moabu wenye wanaponyokaNa kwa ajili ya wale wenye kubakia katika inchi.+