Isaya 3:1-26
3 Kwa maana angalia! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,Anaondoa katika Yerusalemu na katika Yuda kila namna ya tegemeo na akiba,Tegemeo lote la mukate na maji,+
2 Mwanaume mwenye nguvu na mupiganaji-vita,Muamuzi na nabii,+ muaguzi na muzee,
3 Mukubwa wa watu makumi tano (50),+ na mwanaume mwenye kuheshimiwa, na mushauri,Muchawi mwenye kujua sana uchawi, na mutu mwenye kuchezesha nyoka mwenye ufundi.+
4 Nitafanya vijana wadogo kuwa wakubwa wao,Na watu wenye kuyumba-yumba* watawatawala.
5 Watu watakandamizana,Kila mumoja na mwenzake.+
Kijana mudogo atashambulia mwanaume muzee,Na mutu mwenye kuzarauliwa atashindana na mutu mwenye kuheshimiwa.+
6 Kila mumoja atashika ndugu yake katika nyumba ya baba yake, na kusema:
“Wewe uko na nguo ya inje—ukuwe kamanda wetu.
Simamia rundo hili la mabomoko yenye yamepinduliwa.”
7 Lakini siku hiyo atakataa:
“Mimi sitakuwa mufunga-vidonda* wenu;Sina chakula wala nguo katika nyumba yangu.
Musinifanye kuwa kamanda juu ya watu.”
8 Kwa maana Yerusalemu imejikwaa,Na Yuda imeanguka,Kwa sababu wanamupinga Yehova kwa neno na tendo;Wanatenda kwa zarau mbele ya kuwapo kwake kwenye utukufu.*+
9 Namna nyuso zao zinaonekana inashuhudia juu yao,Na wanatangaza zambi yao kama Sodoma;+Hawajaribu kuificha.
Ole wao,* kwa maana wanajiletea musiba!
10 Ambia wenye haki kwamba mambo yatawaendea muzuri;Watapewa zawabu kwa sababu ya mambo yenye wanatenda.*+
11 Ole wake mutu muovu!
Atapatwa na musiba,Kwa maana atatendewa mambo yenye mikono yake imetenda!
12 Na kuhusu watu wangu, wasimamizi wao wa kazi wanawatesa,Na wanamuke wanawatawala.
Watu wangu, viongozi wenu wanafanya mutange-tange,Na wanavuruga muelekeo wa njia zenu.+
13 Yehova anasimama ili kutoa mashitaka;Anasimama ili kutoa hukumu juu ya vikundi vya watu.
14 Yehova ataingia katika hukumu pamoja na wazee na wakubwa wa watu wake.
“Mumeteketeza kwa moto shamba la mizabibu,Na vitu vyenye mumeiba maskini viko katika nyumba zenu.+
15 Namna gani munaweza kuponda watu wangu,Na kusaga nyuso za maskini katika mavumbi?”+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, anasema.
16 Yehova anasema: “Kwa sababu mabinti wa Sayuni ni wenye majivuno,Na wanatembea vichwa vyao vikiwa vimeinuliwa juu,*Wakifinya-finya macho yao kwa kutamani, wakitembea kwa hatua fupifupi,Wakitoa mulio wa kengele kwa mikufu ya kifundo cha miguu yao,
17 Yehova pia atapiga kichwa cha mabinti wa Sayuni kwa vigaga,*Na Yehova atafunua wazi paji la uso wao.+
18 Katika siku hiyo Yehova ataondoa uzuri wa vikomo vyao vya miguu,Tepe za kichwa na mapambo yenye umbo ya mwezi mupya,+
19 Mahereni ya masikio, vikomo, na vitambaa vya kufunika kichwa,
20 Vitambaa vya kichwa, minyororo myembamba ya kifundo cha muguu, na nguo za kifua,*Chupa za marashi* na hirizi,*
21 Pete za vidole na pete za pua,
22 Kanzu za sikukuu, kanzu fupi za inje, nguo za inje, na mifuko,
23 Vioo vya mukono+ na nguo za kitani,*Vilemba na vitambaa vya kufunika kichwa.
24 “Pa nafasi ya mafuta ya zeri,+ kutakuwa harufu ya kuoza;Pa nafasi ya mukaba,* kamba;Pa nafasi ya mutindo muzuri wa nywele, upara;+Pa nafasi ya nguo ya bei kali, nguo ya gunia;+Na kutiwa alama kwenye mwili pa nafasi ya uzuri.
25 Wanaume wako wataanguka kwa upanga,Na wanaume wako wenye nguvu wataanguka katika vita.+
26 Miingilio yake italia na kuomboleza,+Naye atakaa chini akiwa ukiwa.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “wenye hawana musimamo.”
^ Ao “muponyeshaji.”
^ Tnn., “katika macho ya utukufu wake.”
^ Ao “Ole kwa nafsi yao.”
^ Tnn., “watakula matunda ya matendo yao.”
^ Tnn., “wakiwa wamenyoosha shingo (koo).”
^ Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.
^ Ao “vitambaa vya kujifunga kiuno.”
^ Tnn., “Nyumba za nafsi.”
^ Ao “kauri zenye kuvuma ambazo zinatumiwa kama mapambo.”
^ Ao “nguo za ndani.”
^ Ao “mushipi.”