Isaya 4:1-6

  • Wanamuke saba kwa mwanaume mumoja (1)

  • Kile chenye Yehova anachipusha kitakuwa chenye utukufu (2-6)

4  Na wanamuke saba (7) watamushika mwanaume mumoja siku hiyo,+ na kusema: “Tutakula mukate wetu wenyeweNa kuvaa nguo zetu wenyewe;Uturuhusu tu tuitwe kwa jina lakoIli kuiondoa haya yetu.”*+ 2  Siku hiyo kile chenye Yehova anachipusha kitakuwa kizuri sana na chenye utukufu, na mazao ya inchi yatakuwa kitu cha kujivunia na uzuri kwa ajili ya waokokaji wa Israeli.+ 3  Kila mutu mwenye atabakia katika Sayuni na kuachwa katika Yerusalemu ataitwa mutakatifu, wale wote katika Yerusalemu wenye kuandikwa kwa ajili ya uzima.+ 4  Wakati Yehova atasafisha uchafu wa* mabinti wa Sayuni+ na kusafisha umwangaji wa damu wa Yerusalemu kutoka ndani yake kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza kwa moto,*+ 5  juu ya eneo lote la mulima Sayuni na juu ya mahali pa mikusanyiko yake, Yehova ataumba wingu na moshi wakati wa muchana na moto wenye kungaa wenye unawaka usiku;+ kwa maana juu ya utukufu wote kutakuwa mahali pa kujificha. 6  Na kutakuwa kibanda kwa ajili ya kivuli wakati wa muchana kutokana na joto,+ na kwa ajili ya kimbilio na ulinzi kutokana na zoruba na mvua.+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, haya yenye wanapata kwa sababu hawaolewe na hawana watoto.
Tnn., “mavi ya.”
Ao “kuondoa.”