Isaya 32:1-20

  • Mufalme na wakubwa watatawala kwa ajili ya haki ya kweli (1-8)

  • Wanamuke wenye hawahangaike wanaonywa (9-14)

  • Baraka wakati roho itamwangwa (15-20)

32  Angalia! Mufalme+ atatawala kwa ajili ya uadilifu,*+Na wakubwa watatawala kwa ajili ya haki.  2  Na kila mumoja atakuwa kama mahali pa kujificha* kwa sababu ya upepo,Mahali pa kujificha* kwa sababu ya zoruba ya mvua,Kama mito midogo ya maji katika inchi yenye haina maji,+Kama kivuli cha mwamba mukubwa katika inchi yenye kukauka.  3  Kisha macho ya wale wenye kuona hayatafungwa tena,Na masikio ya wale wenye kusikia yatasikiliza.  4  Moyo wa wale wenye kutenda haraka-haraka utafikiri sana* juu ya ujuzi,Na ulimi wa wenye kigugumizi utazungumuza waziwazi na bila kukwama-kwama.+  5  Mutu mwenye hana akili hataitwa tena mukarimu,Na mutu mwenye haongozwe na kanuni hataitwa mwenye cheo;  6  Kwa maana mutu mwenye hana akili atazungumuza kwa upumbavu,Na moyo wake utatunga mambo yenye kuumiza,+Ili kuendeleza uasi-imani* na kusema mambo mapotovu juu ya Yehova,Ili kufanya mwenye njaa abakie* bila kula,Na ili kuima mwenye kiu maji ya kunywa.  7  Mipango ya mutu mwenye haongozwe na kanuni ni mibaya;+Anaendeleza mwenendo wa haya,Ili kumuharibu kwa uongo mutu mwenye kuteseka,+Hata wakati maskini anasema jambo lenye kuwa sawa.  8  Lakini mutu mukarimu iko* na nia ya ukarimu,Na anaendelea kufanya matendo ya ukarimu.*  9  “Ninyi wanamuke wenye hawajali, musimame na musikilize sauti yangu! Ninyi mabinti wenye hawahangaike,+ musikilize kile ninasema! 10  Kisha mwaka mumoja hivi, ninyi wenye hamuhangaike mutatetemeka,Kwa sababu hakuna matunda yenye yatakuwa yamekusanywa wakati mavuno ya zabibu yataisha.+ 11  Mutetemeke, ninyi wanamuke wenye hawajali! Mutetemeke, ninyi wenye hamuhangaike! Muvue nguo na kuwa uchi,Na muvae nguo za magunia kuzunguka viuno vyenu.+ 12  Mupige vifua vyenu kwa kuombolezaKwa sababu ya mashamba yenye kutamanika na muzabibu wenye kuzaa matunda. 13  Kwa maana udongo wa watu wangu utafunikwa kwa miiba na michongoma;Itafunika nyumba zote zenye kushangilia,Ndiyo, muji wenye kushangilia.+ 14  Kwa maana munara wenye ngome umeachwa;Muji wenye makelele umeachwa.+ Ofeli+ na munara wa mulinzi vimekuwa eneo lenye limeachwa siku zote,Mahali kwenye kunapendwa na punda wa pori,Malisho kwa ajili ya makundi,+ 15  Mupaka wakati roho itamwangwa juu yetu kutoka juu,+Na jangwa likuwe shamba la matunda,Na shamba la matunda lionwe kuwa pori.+ 16  Kisha haki itakaa katika jangwa,Na uadilifu* utakaa katika shamba la matunda.+ 17  Matokeo ya haki ya kweli yatakuwa amani,+Na matunda ya haki ya kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.+ 18  Watu wangu watakaa katika makao yenye amani,Katika makao salama na katika mahali pa kupumuzikia penye utulivu.+ 19  Lakini mvua ya majiwe itaangusha pori chini,Na muji utasawazishwa kabisa. 20  Wenye furaha ni ninyi wenye kupanda mbegu pembeni-pembeni ya maji yote,Ninyi wenye kupeleka inje* ngombe-dume na punda.”+

Maelezo ya Chini

Ao “kibanda.”
Ao “Kimbilio.”
Ao “utatafakari.”
Ao “kutenda bila kumuogopa Mungu.”
Ao “nafsi ya mwenye njaa ishinde.”
Ao “eko.”
Ao “matendo ya muzuri.”
Ao “kuachilia.”