Isaya 32:1-20
32 Angalia! Mufalme+ atatawala kwa ajili ya uadilifu,*+Na wakubwa watatawala kwa ajili ya haki.
2 Na kila mumoja atakuwa kama mahali pa kujificha* kwa sababu ya upepo,Mahali pa kujificha* kwa sababu ya zoruba ya mvua,Kama mito midogo ya maji katika inchi yenye haina maji,+Kama kivuli cha mwamba mukubwa katika inchi yenye kukauka.
3 Kisha macho ya wale wenye kuona hayatafungwa tena,Na masikio ya wale wenye kusikia yatasikiliza.
4 Moyo wa wale wenye kutenda haraka-haraka utafikiri sana* juu ya ujuzi,Na ulimi wa wenye kigugumizi utazungumuza waziwazi na bila kukwama-kwama.+
5 Mutu mwenye hana akili hataitwa tena mukarimu,Na mutu mwenye haongozwe na kanuni hataitwa mwenye cheo;
6 Kwa maana mutu mwenye hana akili atazungumuza kwa upumbavu,Na moyo wake utatunga mambo yenye kuumiza,+Ili kuendeleza uasi-imani* na kusema mambo mapotovu juu ya Yehova,Ili kufanya mwenye njaa abakie* bila kula,Na ili kuima mwenye kiu maji ya kunywa.
7 Mipango ya mutu mwenye haongozwe na kanuni ni mibaya;+Anaendeleza mwenendo wa haya,Ili kumuharibu kwa uongo mutu mwenye kuteseka,+Hata wakati maskini anasema jambo lenye kuwa sawa.
8 Lakini mutu mukarimu iko* na nia ya ukarimu,Na anaendelea kufanya matendo ya ukarimu.*
9 “Ninyi wanamuke wenye hawajali, musimame na musikilize sauti yangu!
Ninyi mabinti wenye hawahangaike,+ musikilize kile ninasema!
10 Kisha mwaka mumoja hivi, ninyi wenye hamuhangaike mutatetemeka,Kwa sababu hakuna matunda yenye yatakuwa yamekusanywa wakati mavuno ya zabibu yataisha.+
11 Mutetemeke, ninyi wanamuke wenye hawajali!
Mutetemeke, ninyi wenye hamuhangaike!
Muvue nguo na kuwa uchi,Na muvae nguo za magunia kuzunguka viuno vyenu.+
12 Mupige vifua vyenu kwa kuombolezaKwa sababu ya mashamba yenye kutamanika na muzabibu wenye kuzaa matunda.
13 Kwa maana udongo wa watu wangu utafunikwa kwa miiba na michongoma;Itafunika nyumba zote zenye kushangilia,Ndiyo, muji wenye kushangilia.+
14 Kwa maana munara wenye ngome umeachwa;Muji wenye makelele umeachwa.+
Ofeli+ na munara wa mulinzi vimekuwa eneo lenye limeachwa siku zote,Mahali kwenye kunapendwa na punda wa pori,Malisho kwa ajili ya makundi,+
15 Mupaka wakati roho itamwangwa juu yetu kutoka juu,+Na jangwa likuwe shamba la matunda,Na shamba la matunda lionwe kuwa pori.+
16 Kisha haki itakaa katika jangwa,Na uadilifu* utakaa katika shamba la matunda.+
17 Matokeo ya haki ya kweli yatakuwa amani,+Na matunda ya haki ya kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.+
18 Watu wangu watakaa katika makao yenye amani,Katika makao salama na katika mahali pa kupumuzikia penye utulivu.+
19 Lakini mvua ya majiwe itaangusha pori chini,Na muji utasawazishwa kabisa.
20 Wenye furaha ni ninyi wenye kupanda mbegu pembeni-pembeni ya maji yote,Ninyi wenye kupeleka inje* ngombe-dume na punda.”+
Maelezo ya Chini
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “kibanda.”
^ Ao “Kimbilio.”
^ Ao “utatafakari.”
^ Ao “kutenda bila kumuogopa Mungu.”
^ Ao “nafsi ya mwenye njaa ishinde.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “matendo ya muzuri.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “kuachilia.”