Isaya 51:1-23
51 “Munisikilize, ninyi wenye kufuatilia haki,Ninyi wenye kumutafuta Yehova.
Muangalie mwamba wenye mulichongwa kutoka kwake,Na shimo la kuchimbua ndani majiwe lenye mulichimbuliwa kutoka ndani yake.
2 Muangalie Abrahamu baba yenuNa Sara+ mwenye aliwazaa.*
Kwa maana alikuwa mumoja wakati nilimuita,+Na nilimubariki na kumufanya kuwa wengi.+
3 Kwa maana Yehova atamufariji Sayuni.+
Atafariji mabomoko yake yote,+Na atafanya jangwa lake kuwa kama Edeni+Na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.+
Kutakuwa furaha na kushangilia ndani yake,Kutoa shukrani na wimbo mutamu.+
4 Munikazie uangalifu, Enyi watu wangu,Na munitegee sikio, taifa langu.+
Kwa maana sheria itatoka kwangu,+Na nitafanya haki yangu kuwa mwangaza kwa vikundi vya watu.+
5 Haki yangu inakaribia.+
Wokovu wangu utatoka,+Na mikono yangu itahukumu vikundi vya watu.+
Visiwa vitanitumainia,+Na vitangojea mukono wangu.*
6 Muinue macho yenu kuelekea mbinguni,Na muangalie chini katika dunia.
Kwa maana mbingu zitasambaa vipande-vipande kama moshi;Na dunia itazeeka kama nguo,Na wakaaji wake watakufa kama imbu.
Lakini wokovu wangu utadumu milele,+Na haki yangu haitashindwa* hata kidogo.+
7 Munisikilize, ninyi wenye kujua haki,Watu wenye kuwa na sheria yangu* katika moyo wao.+
Musiogope zihaka za wanadamu wenye wanaweza kufa,Na musiogope kwa sababu ya matusi yao.
8 Kwa maana nondo* atawakula kama vile nguo;Nondo* wa nguo atawakula kama manyoya ya kondoo.+
Lakini haki yangu itadumu milele,Na wokovu wangu kwa vizazi vyote.”+
9 Amuka! Amuka! Uvae nguvu,Ee mukono wa Yehova!+
Amuka kama katika siku za zamani sana, kama katika vizazi vyenye vilipita.
Je, haiko wewe ndiye ulivunja Rahabu*+ vipande-vipande,Mwenye ulitoboa kwa silaha ule munyama mukubwa wa bahari?+
10 Je, haiko wewe ndiye ulikausha bahari, maji ya sehemu yenye kuenda chini sana?+
Mwenye ulifanya sehemu za chini kabisa za bahari kuwa njia ili watu wenye walikombolewa wavuke?+
11 Watu wa Yehova wenye walikombolewa watarudia.+
Watakuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe,+Na shangwe yenye haina mwisho itakuwa taji lao.*+
Watakuwa na furaha na shangwe.
Na huzuni na kilio cha maumivu vitakimbia.+
12 “Mimi mwenyewe ndiye Mwenye kuwafariji.+
Sababu gani uogope mwanadamu mwenye anaweza kufa mwenye atakufa,+Na mwana wa binadamu mwenye atakauka kama majani ya mubichi?
13 Sababu gani unamusahau Yehova Mutengenezaji wako,+Mwenye alitandika mbingu+ na kuweka musingi wa dunia?
Na muchana wote uliendelea kuogopa kila wakati kasirani kali ya mukandamizaji,*Kama vile alikuwa tayari kukuharibu.
Iko wapi sasa, kasirani kali ya mukandamizaji?
14 Ule mwenye kuinama katika minyororo atawekwa huru hivi karibuni;+Hatakufa na kuingia katika shimoWala hatakosa mukate.
15 Lakini mimi ni Yehova Mungu wako,Mwenye anachafua bahari na kufanya mawimbi yake yakuwe na muchafuko+—Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+
16 Nitatia maneno yangu katika kinywa chako,Na nitakufunika kwa kivuli cha mukono wangu,+Ili kupanda mbingu na kuweka musingi wa dunia+Na kuambia Sayuni, ‘Muko watu wangu.’+
17 Amuka! Amuka! Simama, Ee Yerusalemu,+Wewe mwenye umekunywa katika mukono wa Yehova kikombe chake cha kasirani kali.
Umekunywa bilauri;Umemaliza kikombe chenye kuleta kuyumba-yumba.+
18 Hakuna hata mumoja wa wana wake wote wenye alizaa mwenye iko* pale ili kumuongozaNa hakuna hata mumoja wa wana wake wenye alilea mwenye amemushika mukono.
19 Mambo hayo mbili yamekupata.
Ni nani atakusikilia huruma?
Uharibifu na maangamizi, njaa na upanga!+
Ni nani atakufariji?+
20 Wana wako wamezimia.+
Wamelala chini kwenye kila makutano ya barabara*Kama kondoo wa pori katika wavu*Wamejaa kasirani kali ya Yehova, kemeo la Mungu wako.”
21 Kwa hiyo tafazali sikiliza jambo hili,Ee mwanamuke mwenye kuteseka na kulewa, hata kama haiko kwa sababu ya divai.
22 Yehova Bwana wako, Mungu wako mwenye kutetea watu wake, anasema hivi:
“Angalia! Nitakamata katika mukono wako kile kikombe chenye kuleta kuyumba-yumba,+Ile bilauri, kikombe changu cha kasirani kali;Hautakikunywa tena.+
23 Nitakitia katika mukono wa wale wenye kukutesa,+Wale wenye walikuambia,* ‘Inama ili tutembee juu yako!’
Basi ukafanya mugongo wako ukuwe kama udongo,Kama barabara yao ya kutembea juu yake.”
Maelezo ya Chini
^ Ao “mwenye aliwazaa kwa maumivu ya kuzaa.”
^ Ao “nguvu zangu.”
^ Ao “haitavunjwa.”
^ Ao “agizo langu.”
^ Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
^ Ao pengine, “Munyoo.”
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “itakuwa juu ya kichwa chao.”
^ Ao “mwenye kukufungia ndani.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “kwenye kichwa cha barabara zote.”
^ Ao “makila.”
^ Ao “waliambia nafsi yako.”