Isaya 6:1-13

  • Katika maono, Isaya anamuona Yehova katika hekalu lake (1-4)

    • “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova” (3)

  • Midomo ya Isaya inasafishwa (5-7)

  • Isaya anatumwa (8-10)

    • “Mimi huyu! Unitume mimi!” (8)

  • “Mupaka wakati gani, Ee Yehova?” (11-13)

6  Katika mwaka wenye Mufalme Uzia alikufa,+ nilimuona Yehova akiwa amekaa kwenye kiti cha ufalme chenye kuwa juu na chenye kuinuliwa,+ na pindo za kanzu lake zilijaza hekalu. 2  Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mumoja wao alikuwa na mabawa sita (6). Kila mumoja* alifunika uso wake kwa mabawa mbili na alifunika miguu yake kwa mabawa mbili, na kila mumoja wao aliruka huku na huku kwa mabawa mbili.  3  Na mumoja aliambia mwenzake: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova wa majeshi.+ Dunia yote inajaa utukufu wake.” 4  Na viegemeo vya vizingiti* vikatetemeka kutokana na ile sauti kubwa,* na nyumba ikajaa moshi.+  5  Kisha nikasema: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimekufa,*Kwa maana mimi ni mutu mwenye hana midomo safi,Na ninaishi kati ya watu wenye hawana midomo safi;+Kwa maana macho yangu yamemuona Mufalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!” 6  Basi, mumoja wa maserafi akaruka ili kuja karibu na mimi, na katika mukono wake alikuwa na kaa la moto+ lenye alikuwa amekamata kwa koleo* kwenye mazabahu.+ 7  Akagusa kinywa changu na kusema: “Angalia! Hili limegusa midomo yako. Hatia yako imeondolewa,Na zambi yako imefunikwa.” 8  Kisha nikasikia sauti ya Yehova akisema: “Nitatuma nani, na ni nani ataenda kwa ajili yetu?”+ Na mimi nikasema: “Mimi huyu! Unitume mimi!”+  9  Naye akajibu: “Uende, na uambie watu hawa: ‘Mutasikia tena na tena,Lakini hamutaelewa;Mutaona tena na tena,Lakini hamutapata ujuzi wowote.’+ 10  Fanya moyo wa watu hawa kuwa mugumu,+Fanya masikio yao kuwa mazito,+Na ufanye macho yao yashikane pamoja,Ili wasione kwa macho yaoNa wasisikie kwa masikio yao,Ili moyo wao usieleweNa ili wasigeuke na kupona.”+ 11  Basi nikasema: “Mupaka wakati gani, Ee Yehova?” Kisha akasema: “Mupaka miji ibomoke na kuwa mabomoko yenye haina mukaajiNa nyumba zikuwe bila watu,Na inchi iharibiwe na kuwa ukiwa;+ 12  Mupaka Yehova aondoe watu na kuwapeleka mbali+Na mupaka hali ya kuachwa ukiwa ya inchi ienee sana. 13  “Lakini bado kutakuwa sehemu moja ya kumi (1/10) ndani yake, na itateketezwa tena kwa moto, kama muti mukubwa na kama muti wa mwaloni, yenye kisha kukatwa inaacha kisiki; mbegu takatifu* itakuwa kisiki chake.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Yeye.”
Hapa kizingiti ni ubao wenye kuwa chini ya mulango.
Tnn., “sauti ya ule mwenye alikuwa anaita.”
Tnn., “nimenyamazishwa.”
Koleo ni kifaa cha kushikia vitu.
Ao “uzao mutakatifu.”