Isaya 6:1-13
6 Katika mwaka wenye Mufalme Uzia alikufa,+ nilimuona Yehova akiwa amekaa kwenye kiti cha ufalme chenye kuwa juu na chenye kuinuliwa,+ na pindo za kanzu lake zilijaza hekalu.
2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mumoja wao alikuwa na mabawa sita (6). Kila mumoja* alifunika uso wake kwa mabawa mbili na alifunika miguu yake kwa mabawa mbili, na kila mumoja wao aliruka huku na huku kwa mabawa mbili.
3 Na mumoja aliambia mwenzake:
“Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova wa majeshi.+
Dunia yote inajaa utukufu wake.”
4 Na viegemeo vya vizingiti* vikatetemeka kutokana na ile sauti kubwa,* na nyumba ikajaa moshi.+
5 Kisha nikasema: “Ole wangu!
Kwa maana ni kama nimekufa,*Kwa maana mimi ni mutu mwenye hana midomo safi,Na ninaishi kati ya watu wenye hawana midomo safi;+Kwa maana macho yangu yamemuona Mufalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!”
6 Basi, mumoja wa maserafi akaruka ili kuja karibu na mimi, na katika mukono wake alikuwa na kaa la moto+ lenye alikuwa amekamata kwa koleo* kwenye mazabahu.+
7 Akagusa kinywa changu na kusema:
“Angalia! Hili limegusa midomo yako.
Hatia yako imeondolewa,Na zambi yako imefunikwa.”
8 Kisha nikasikia sauti ya Yehova akisema: “Nitatuma nani, na ni nani ataenda kwa ajili yetu?”+ Na mimi nikasema: “Mimi huyu! Unitume mimi!”+
9 Naye akajibu: “Uende, na uambie watu hawa:
‘Mutasikia tena na tena,Lakini hamutaelewa;Mutaona tena na tena,Lakini hamutapata ujuzi wowote.’+
10 Fanya moyo wa watu hawa kuwa mugumu,+Fanya masikio yao kuwa mazito,+Na ufanye macho yao yashikane pamoja,Ili wasione kwa macho yaoNa wasisikie kwa masikio yao,Ili moyo wao usieleweNa ili wasigeuke na kupona.”+
11 Basi nikasema: “Mupaka wakati gani, Ee Yehova?” Kisha akasema:
“Mupaka miji ibomoke na kuwa mabomoko yenye haina mukaajiNa nyumba zikuwe bila watu,Na inchi iharibiwe na kuwa ukiwa;+
12 Mupaka Yehova aondoe watu na kuwapeleka mbali+Na mupaka hali ya kuachwa ukiwa ya inchi ienee sana.
13 “Lakini bado kutakuwa sehemu moja ya kumi (1/10) ndani yake, na itateketezwa tena kwa moto, kama muti mukubwa na kama muti wa mwaloni, yenye kisha kukatwa inaacha kisiki; mbegu takatifu* itakuwa kisiki chake.”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Yeye.”
^ Hapa kizingiti ni ubao wenye kuwa chini ya mulango.
^ Tnn., “sauti ya ule mwenye alikuwa anaita.”
^ Tnn., “nimenyamazishwa.”
^ Koleo ni kifaa cha kushikia vitu.
^ Ao “uzao mutakatifu.”