Isaya 34:1-17

  • Kisasi cha Yehova juu ya mataifa (1-8)

  • Edomu itafanywa kuwa ukiwa (9-17)

34  Mukuje karibu ili musikie, ninyi vikundi vya watu,Na mukaze uangalifu, ninyi watu,Dunia na vyote vyenye kuijaza visikilize,Inchi na mazao yake yote.  2  Kwa maana kasirani kali ya Yehova iko juu ya mataifa yote,+Na gazabu yake iko juu ya jeshi lao lote.+ Na atawaharibu;Atawatoa ili wauawe.+  3  Watu wao wenye waliuawa watatupwa inje,Na harufu ya mubaya ya mizoga yao itapanda;+Milima itayeyuka kwa sababu ya* damu yao.+  4  Jeshi lote la mbinguni litaoza,Na mbingu zitakunjwa kama kitabu cha kukunjwa. Jeshi lao lote litakauka,Kama vile jani lenye kukauka linaanguka kutoka kwenye muzabibuNa tini yenye kukauka kutoka kwenye muti wa tini.  5  “Kwa maana upanga wangu utalowanishwa mbinguni.+ Utashuka juu ya Edomu katika hukumu+Juu ya watu wenye nimeamua kuharibu.  6  Yehova iko* na upanga; utafunikwa kwa damu. Utafunikwa kwa mafuta,+Kwa damu ya wana-kondoo na mbuzi,Kwa mafuta ya figo za kondoo-dume. Kwa maana Yehova iko* na zabihu katika Bosra,Machinjo makubwa katika inchi ya Edomu.+  7  Ngombe-dume wa pori watashuka pamoja nao,Ngombe-dume wadogo pamoja na wenye nguvu. Inchi yao itajaa damu,Na mavumbi yao yatalowanishwa kwa mafuta.”  8  Kwa maana Yehova iko* na siku ya kisasi,+Mwaka wa malipo kwa ajili ya kesi ya hukumu juu ya Sayuni.+  9  Mito yake ya kidogo* itabadilishwa kuwa kabulimbo,Na mavumbi yake kuwa kiberiti,Na inchi yake itakuwa kama lami yenye kuwaka. 10  Haitazimishwa usiku wala muchana;Moshi wake utaendelea kupanda milele. Atabakia mwenye kuharibiwa kizazi kwa kizazi;Hakuna mwenye atapita katikati yake milele na milele.+ 11  Mwari na nungunungu watamuriti,Na bundi wenye masikio ya murefu na kunguru watakaa ndani yake. Atanyoosha juu yake kamba ya kupimia ya uwaziNa kamba ya kupima usawa* ya uharibifu. 12  Hakuna mutu kati ya watu wake wenye vyeo mwenye atafanywa kuwa mufalme,Na wakubwa wake wote watakuwa bure. 13  Miiba itatokea katika minara yake yenye ngome,Mimea yenye kuwasha na magugu yenye miiba katika mahali pake penye ngome. Atakuwa pango la mbweha,+Kiwanja cha mbuni. 14  Viumbe vya jangwa vitakutana na wanyama wenye kulia,Na mbuzi wa pori* atamuita mwenzake. Ndiyo, pale babewana atakaa na kupata mahali pa kupumuzikia. 15  Nyoka-pili atatengeneza nyumba yake pale na kutaga mayai,Na atayatotoa na kukusanya vitoto katika kivuli chake. Ndiyo, kipanga watakusanyika pale, kila mumoja na mwenzake. 16  Mutafute katika kitabu cha Yehova na mukisome kwa sauti kubwa: Hakuna hata mumoja wao mwenye atakosekana;Hakuna hata mumoja wao mwenye atakosa mwenzake,Kwa maana kinywa cha Yehova ndicho kimeamuru,Na roho yake ndiyo imewakusanya pamoja. 17  Yeye ndiye amewapigia kura,Na mukono wake mwenyewe umewapimia mahali kwenye wamegawiwa.* Watapariti kwa wakati wote;Watakaa ndani yake kwa vizazi vyote.

Maelezo ya Chini

Ao “itatiririka.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Inaonekana ni mito midogo ya Bosra, muji mukubwa wa Edomu.
Tnn., “majiwe.”
Ao pengine, “pepo muchafu mwenye kufanana na mbuzi.”
Tnn., “amewagawia hiyo kwa kamba ya kupimia.”