Isaya 38:1-22
38 Katika siku hizo Hezekia akakuwa mugonjwa na alikuwa karibu kufa.+ Nabii Isaya+ mwana wa Amozi akakuja na kumuambia, “Yehova anasema hivi: ‘Patia nyumba yako maagizo, kwa maana utakufa; hautapona.’”+
2 Basi Hezekia akageuza uso wake kuelekea ukuta na kuanza kusali kwa Yehova:
3 “Ninakuomba, Ee Yehova, kumbuka,+ tafazali, namna nimetembea mbele yako kwa uaminifu na kwa moyo kamili,+ na nimetenda mambo mema mbele ya macho yako.” Na Hezekia akaanza kulia sana.
4 Kisha neno la Yehova likakuja kwa Isaya, na kusema:
5 “Rudia na umuambie Hezekia,+ ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako anasema hivi: “Nimesikia sala yako.+ Nimeona machozi yako.+ Angalia, ninaongeza miaka kumi na tano (15) kwenye maisha yako,*+
6 na nitakuokoa wewe na muji huu kutoka katika mukono wa mufalme wa Ashuru, na nitalinda muji huu.+
7 Hii ndiyo alama kutoka kwa Yehova yenye itakuonyesha kwamba Yehova atatimiza neno lenye amesema:+
8 Nitafanya kivuli cha jua chenye kushuka kwenye ngazi* ya Ahazi kirudie nyuma hatua kumi (10).”’”+ Basi jua likarudia nyuma hatua kumi kwenye ngazi zenye tayari lilikuwa limeshuka.
9 Haya ni maandishi ya* Mufalme Hezekia wa Yuda, wakati alishikwa na ugonjwa na kupona ugonjwa wake.
10 Nilisema: “Katikati ya maisha yanguLazima niingie katika milango mikubwa ya Kaburi.*
Nitaimwa miaka yangu yenye inabakia.”
11 Nilisema: “Sitamuona Yah,* Yah katika inchi ya wazima.+
Sitaona tena wanadamuWakati nitakuwa pamoja na wakaaji wa mahali kwenye kila kitu kinafikia mwisho.
12 Makao yangu yamengolewa na kupelekwa mbali na mimi+Kama hema ya muchungaji.
Nimekunja uzima wangu kama musukaji wa nguo;Ananikata kama nyuzi za murefu zenye kutoka juu kuenda chini.*
Kuanzia mapambazuko* mupaka wakati giza linaingia unaendelea kunileta kwenye mwisho.+
13 Nimejituliza mupaka asubui.
Kama simba, anaendelea kuvunja mifupa yangu yote;Kuanzia mapambazuko* mupaka wakati giza linaingia unaendelea kunileta kwenye mwisho.+
14 Ninaendelea kulia kama ndege teleka ao ndege kuruwiji;*+Ninaendelea kulia kama njiwa.+
Macho yangu yameangalia nafasi ya juu kwa uchovu:+
‘Ee Yehova, niko katika taabu kubwa;Unisaidie.’*+
15 Niseme nini?
Amezungumuza na mimi na kutenda.
Nitatembea kwa unyenyekevu* miaka yangu yoteKwa sababu ya uchungu wangu mwingi.*
16 ‘Ee Yehova, kila mwanadamu anaishi kwa mambo hayo,*Na uzima wa roho yangu uko katika mambo hayo.
Utanirudishia afya ya muzuri na kulinda uzima wangu.+
17 Angalia! Kuliko kuwa na amani, nilikuwa na uchungu mwingi;Lakini kwa sababu ulinipenda sana*Ulinilinda nisiingie katika shimo la uharibifu.+
Kwa maana umetupa zambi zangu zote nyuma ya mugongo wako.*+
18 Kwa maana Kaburi* haliwezi kukutukuza,+Kifo hakiwezi kukusifu.+
Wale wenye kushuka katika shimo hawawezi kutumainia uaminifu wako.+
19 Wazima, wazima wanaweza kukusifu,Kama vile ninaweza kukusifu leo hii.
Baba anaweza kupatia wana wake ujuzi kuhusu uaminifu wako.+
20 Ee Yehova, uniokoeNa tutapiga nyimbo zangu kwa vyombo vya kamba+Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+
21 Kisha Isaya akasema: “Mulete keki ya tini zenye kukauka zenye zilifinywa-finywa na muitie kwenye jipu hilo, ili apone.”+
22 Hezekia alikuwa ameuliza: “Ni nini alama ya kwamba nitapanda kuenda kwenye nyumba ya Yehova?”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “siku zako.”
^ Pengine ngazi hizo zilitumiwa ili kuhesabia wakati, kama saa ya kivuli.
^ Ao “utungo wa.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
^ Ao “nyuzi za mutanda.” Angalia Maana ya Maneno.
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Ao pengine, “korongo.”
^ Tnn., “Ukuwe uhakika wangu.”
^ Ao “kwa heshima.”
^ Ao “uchungu wa nafsi yangu.”
^ Ni kusema, maneno na matendo ya Mungu.
^ Ao “umeondoa zambi zangu zote mbele ya macho yako.”
^ Ao “ulipenda nafsi yangu.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

