Isaya 45:1-25

  • Koreshi anachaguliwa ili kukamata Babiloni (1-8)

  • Udongo haupaswe kushindana na Mufinyanzi (9-13)

  • Mataifa mengine yanatambua Israeli (14-17)

  • Mungu ni mwenye kutegemeka katika uumbaji na katika kufunua mambo (18-25)

    • Dunia iliumbwa ili ikaliwe na watu (18)

45  Yehova anamuambia hivi mutiwa-mafuta wake, Koreshi,+Mwenye nimeshika mukono wake wa kuume,+Ili kutiisha mataifa mbele yake,+Kunyanganya wafalme silaha,*Kufungua mbele yake milango yenye pande mbili,Na hivyo milango mikubwa haitafungwa:  2  “Nitaenda mbele yako,+Na nitasawazisha vilima. Nitavunja milango ya shaba vipande-vipande,Na nitakata mapingo* ya chuma.+  3  Nitakupatia hazina zenye kuwa katika gizaNa hazina zenye kufichwa katika mahali kwenye kufichwa,+Ili ujue kwamba mimi ni Yehova,Mungu wa Israeli, mwenye kukuita kwa jina lako.+  4  Kwa ajili ya mutumishi wangu Yakobo na Israeli muchaguliwa wangu,Ninakuita kwa jina lako. Ninakupatia jina la heshima, hata kama haukunijua.  5  Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote. Hakuna Mungu isipokuwa mimi.+ Nitakutia nguvu,* hata kama haukunijua,  6  Ili watu wajueKuanzia mahali jua linatokea mupaka mahali jua linashukia*Kwamba hakuna mwingine isipokuwa mimi.+ Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.+  7  Ninafanya mwangaza+ na kuumba giza,+Ninafanya amani+ na kuumba musiba;+Mimi, Yehova, ninafanya mambo hayo yote.  8  “Ninyi mbingu, munyeshe mvua kutoka juu;+Mawingu yatiririshe haki. Dunia ifunguke na izae wokovu,Na ichipushe haki wakati uleule.+ Mimi, Yehova, nimeiumba.”  9  Ole wake ule mwenye kushindana* na Mutengenezaji wake,*Kwa maana yeye ni kipande tu cha chombo cha udongoKati ya vipande vingine vya chombo cha udongo vyenye kuwa chini! Je, udongo utamuambia mufinyanzi:* “Unatengeneza nini?”+ Ao kitu chenye ulitengeneza kiseme: “Yeye hana mikono”?* 10  Ole wake mwenye anamuambia baba: “Wewe umezaa nini?” Na kumuambia mwanamuke: “Unazaa nini?”* 11  Yehova, Mutakatifu wa Israeli+ na Mufanyizaji wake, anasema hivi: “Je, mutaniuliza kuhusu mambo yenye kujaNa kuniamuru kuhusu wana wangu+ na kuhusu kazi za mikono yangu? 12  Nilifanya dunia+ na kumuumba mwanadamu juu yake.+ Nilitandika mbingu kwa mikono yangu mwenyewe,+Na ninapatia jeshi lake lote maagizo.”+ 13  “Nimemuinua mutu katika haki,+Na nitanyoosha njia zake zote. Yeye ndiye atajenga muji wangu,+Na kuweka huru+ bila bei ao rushwa* watu wangu wenye wamepelekwa katika uhamisho,”+ ni vile Yehova wa majeshi anasema. 14  Yehova anasema hivi: “Faida ya* Misri na vitu vya biashara vya* Etiopia na Wasabea, watu warefu,Watakuja kwako na kuwa wako. Watatembea nyuma yako wakiwa na minyororo. Watakuja na kukuinamia.+ Watasali kwako wakisema, ‘Kwa kweli Mungu iko* pamoja na wewe,+Na hakuna mwingine yeyote; hakuna Mungu mwingine.’” 15  Kwa kweli wewe ni Mungu mwenye kujificha,Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi.+ 16  Wote watapatishwa haya na kufezeheshwa;Watengenezaji wote wa sanamu wataondoka na haya.+ 17  Lakini Israeli ataokolewa na Yehova kwa wokovu wa milele.+ Hamutapatishwa haya wala kufezeheshwa kwa umilele wote.+ 18  Kwa maana Yehova,Muumbaji wa mbingu,+ Mungu wa kweli,Mwenye alifanya dunia, Mutengenezaji wake mwenye aliifanya imara kabisa,+Mwenye hakuiumba tu bila sababu,* lakini aliifanya ili ikaliwe na watu, anasema hivi:+ “Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine. 19  Sikusema katika mahali kwenye kufichwa,+ katika inchi yenye giza;Sikuambia uzao wa* Yakobo,‘Munitafute tu bila sababu.’* Mimi ni Yehova, mwenye kusema mambo ya haki na kutangaza mambo ya unyoofu.+ 20  Mukusanyike pamoja na mukuje. Mukaribie pamoja, ninyi wenye muliponyoka kutoka kwa mataifa.+ Wale wenye kubeba sanamu za kuchonga hawajue kituNa wanasali kwa mungu mwenye hawezi kuwaokoa.+ 21  Mutoe ripoti yenu, mulete kesi yenu ya hukumu. Wapatiane mawazo kwa umoja. Ni nani alitabiri jambo hili zamani sana? Na kulitangaza tangu nyakati zenye zilipita? Je, haiko mimi, Yehova? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi;Mungu mwenye haki na Mwokozi,+ hakuna mwingine isipokuwa mimi.+ 22  Mugeuke mukuje kwangu na muokolewe,+ miisho yote ya dunia,Kwa maana mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.+ 23  Nimeapa kwa jina langu;Neno limetoka katika kinywa changu katika haki,Na halitarudia:+ Kila goti litapigwa mbele yangu,Kila ulimi utaapa ushikamanifu+ 24  Na useme, ‘Hakika katika Yehova kuko haki ya kweli na nguvu. Wale wote wenye kumukasirikia watakuja mbele yake wakiwa na haya. 25  Katika Yehova uzao wote wa Israeli utaonekana* kuwa sawa+Na watajisifu katika yeye.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “kufungua viuno vya wafalme.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “Nitakufunga sana kiuno.”
Ao “kuanzia mashariki mupaka mangaribi.”
Ao “kubishana.”
Ao “na Ule mwenye alimufanya.”
Ao “Ule mwenye aliufanya.”
Ao pengine, “Je, udongo unapaswa kusema: ‘Kazi yako haina vishikio’?”
Ao “Uko na uchungu wa kuzaa nini?”
Ao “kata-midomo.”
Ao pengine, “Wafanyakazi wa.”
Ao pengine, “wafanyabiashara wa.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “ili ibakie wazi.”
Tnn., “mbegu ya.”
Ao “bure.”
Tnn., “mbegu yote ya Israeli itaonekana.”