Isaya 13:1-22
13 Tangazo juu ya Babiloni+ lenye Isaya+ mwana wa Amozi aliona katika maono:
2 “Musimamishe alama*+ juu ya mulima wa miamba yenye haina kitu.
Muwaite kwa sauti kubwa, mupepee mukono,Ili waingie katika miingilio ya watu wenye vyeo.
3 Nimetoa amri kwa wale wenye nimeweka katika madaraka.*+
Nimeita wapiganaji-vita wangu ili kuonyesha kasirani yangu,Watu wangu wenye kushangilia kwa kujivuna.
4 Musikilize! Kikundi cha watu katika milima;Ni kama sauti ya watu wengi sana!
Musikilize! Fujo za falme,Za mataifa yenye kukusanyika pamoja!+
Yehova wa majeshi anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.+
5 Wanakuja kutoka inchi ya mbali,+Kutoka mwisho wa mbingu,Yehova na silaha za kasirani yake kali,Ili kuharibu dunia yote.+
6 Muomboleze, kwa maana siku ya Yehova iko karibu!
Itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mweza-Yote.+
7 Ndiyo sababu mikono yote itaregea,Na moyo wa kila mwanadamu utayeyuka kwa woga.+
8 Watu wamekuwa na wasiwasi.+
Wameshikwa na uchungu na maumivu,Kama mwanamuke mwenye kuzaa.
Wanaangaliana kwa woga mukubwa,Wakiwa na nyuso zenye kuwaka kwa uchungu.
9 Angalia! Siku ya Yehova inakuja,Ikiwa na ukali na kasirani kali na hasira yenye kuwaka,Ili kufanya inchi kuwa kitu cha kuogopesha sana,+Na kuharibu watenda-zambi wa inchi wasikuwe tena ndani yake.
10 Kwa maana nyota za mbinguni na makundi yake ya nyota*+Havitatoa mwangaza wavyo;Jua litakuwa na giza wakati litatokea,Na mwezi hautatoa mwangaza wake.
11 Nitaomba dunia yenye kuikaliwa na watu itoe hesabu kwa sababu ya ubaya wake,+Na waovu kwa sababu ya kosa lao.
Nitamaliza kiburi cha wenye kimbelembele,Na nitashusha kiburi cha wenye kuonea.+
12 Nitafanya mwanadamu mwenye anaweza kufa akosekane kuliko zahabu yenye kusafishwa,+Na wanadamu wakosekane kuliko zahabu ya Ofiri.+
13 Ndiyo maana nitafanya mbingu zitetemekeNa dunia itatikiswa na kutoka mahali pake+Kwa sababu ya kasirani kali ya Yehova wa majeshi katika siku ya hasira yake yenye kuwaka.
14 Kama swala mwenye kuwindwa na kama kundi lenye halina mutu wa kulikusanyaKila mumoja atarudia kwa watu wake;Kila mumoja atakimbia kuenda kwenye inchi yake mwenyewe.+
15 Kila mutu mwenye atapatikana atatobolewa kwa silaha,Na kila mutu mwenye atakamatwa ataanguka kwa upanga.+
16 Watoto wao watavunjwa vipande-vipande mbele ya macho yao,+Vitu vya nyumba zao vitanyanganywa,Na bibi zao watalalwa kinguvu.
17 Angalia, ninasimamisha Wamedi+ ili wapigane nao,Wenye hawaone feza kuwa kituNa wenye hawafurahie zahabu.
18 Pinde zao zitavunja-vunja vijana wanaume;+Hawatasikilia huruma uzao wa tumbo la uzazi;Wala kuonyesha watoto rehema.
19 Na Babiloni, ufalme wenye utukufu zaidi,*+Uzuri na kiburi cha Wakaldayo,+Itakuwa kama wakati Mungu alipindua Sodoma na Gomora.+
20 Haitaikaliwa na watu hata siku moja,Wala haitakuwa mahali pa kuishi kwa vizazi vyote.+
Hakuna Mwarabu mwenye atasimamisha hema yake kule,Na hakuna wachungaji wenye watapumuzisha makundi yao kule.
21 Viumbe vya jangwa vitalala kule;Nyumba zao zitajaa bundi-tai.
Mbuni watakaa kule,+Na mbuzi wa pori* watarukaruka kule.
22 Wanyama wenye kulia watalia katika minara yake,Na mbweha katika makao yake yenye kupendeza sana.
Wakati wake umekaribia, na siku zake hazitarefushwa.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Tnn., “kwa watu wangu wenye kutakaswa.”
^ Tnn., “na Kesili zao,” pengine ni kundi la nyota la Orioni na makundi ya nyota yenye kulizunguka.
^ Ao “pambo la falme.”
^ Ao pengine, “Na pepo wachafu wenye kufanana na mbuzi.”