Isaya 18:1-7
-
Ujumbe juu ya Etiopia (1-7)
18 Ole wake inchi ya vidudu vyenye mabawa yenye kuvuma,Katika eneo la mito ya Etiopia!+
2 Inatuma wajumbe kupitia bahari,Wenye wanavuka maji katika vyombo vya mafunjo,* na kusema:
“Muende, ninyi wajumbe wenye kuenda haraka,Kwa taifa lenye watu warefu na wenye ngozi laini,*Kwa watu wenye kuogopwa kila mahali,+Kwa taifa lenye nguvu, lenye kushinda,*Lenye inchi yake imefagiliwa mbali na mito.”
3 Ninyi wakaaji wote wa inchi na ninyi wakaaji wa dunia,Kile mutaona kitakuwa kama alama* yenye kuinuliwa juu ya milima,Na mutasikia sauti kama ya baragumu yenye kupigwa.
4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi:
“Nitaendelea kutulia na kuangalia* mahali pangu penye pamefanywa kuwa imaraKama joto lenye kumeremeta pamoja na mwangaza wa jua,Kama wingu la umande katika joto la mavuno.
5 Kwa maana mbele ya mavuno,Wakati ua linakamilika na kuwa zabibu yenye kukomaa,Machipukizi yake yatakatwa kwa miunduVikonyo* vitakatwa na kuondolewa.
6 Wote wataachiwa ndege wenye kuwinda wa milimaNa wanyama wa dunia.
Ndege wenye kuwinda watakaa juu yao wakati wa kipindi cha joto,Na wanyama wote wa dunia watakaa juu yao wakati wa mavuno.
7 Wakati huo zawadi italetwa kwa Yehova wa majeshi,Kutoka kwa taifa lenye watu warefu na wenye ngozi laini,*Kutoka kwa watu wenye kuogopwa kila mahali,Kutoka kwa taifa lenye nguvu, lenye kushinda,*Lenye inchi yake imefagiliwa mbali na mito,Mupaka mahali kwenye kunabeba jina la Yehova wa majeshi, Mulima Sayuni.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “papyrus.” Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “taifa lenye kurefushwa na kusuguliwa.”
^ Ao “taifa lenye nguvu nyingi lenye linakanyanga-kanyanga.”
^ Ao “nguzo ya alama.”
^ Ao pengine, “kuangalia nikiwa.”
^ Kikonyo ni sehemu ya mumea yenye inashikilia kwenye kitu kingine kwa kujiviringa-viringa.
^ Tnn., “taifa lenye kurefushwa na kusuguliwa.”
^ Ao “taifa lenye nguvu nyingi lenye linakanyanga-kanyanga.”