Isaya 64:1-12

  • Sala ya kutubu inaendelea (1-12)

    • Yehova “Mufinyanzi wetu” (8)

64  Kama tu ungepasua mbingu na kushuka chini,Ili milima itetemeke kwa sababu yako,  2  Kama vile wakati moto unawasha miti midogo-midogo,Na moto unafanya maji yatokote,Basi jina lako lingejulikana kwa wapinzani wako,Na mataifa yangetetemeka mbele yako!  3  Wakati ulifanya mambo ya kuogopesha yenye hatukupima kutazamia,+Ulishuka, na milima ilitetemeka mbele yako.+  4  Tangu zamani hakuna mwenye alisikia wala kutega sikio,Wala hakuna jicho lenye lilimuona Mungu isipokuwa wewe,Mwenye kutenda kwa ajili ya wale wenye wanaendelea kumungojea.*+  5  Umekutana na wale wenye wanafurahia kutenda mambo yenye kuwa sawa,+Wale wenye wanakukumbuka na kufuata njia zako. Angalia! Ulikuwa na kasirani kali, wakati huo sisi tuliendelea kutenda zambi,+Tulifanya vile kwa wakati murefu. Je, sasa tuokolewe?  6  Na sisi wote tumekuwa kama mutu mwenye haiko safi,Na matendo yetu yote ya haki yako kama kipande cha nguo chenye mwanamuke anatumia katika siku zake za kuona mwezi.*+ Sisi wote tutakauka kama jani,Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.  7  Hakuna mwenye anaitia jina lako,Hakuna mwenye anajikaza kukushika,Kwa maana umetuficha uso wako,+Na unafanya tukuwe wazaifu* kwa sababu ya* kosa letu.  8  Lakini sasa, Ee Yehova, uko Baba yetu.+ Tuko udongo, na wewe uko Mufinyanzi wetu;*+Sisi wote tuko kazi ya mukono wako.  9  Usikasirike sana, Ee Yehova,+Na usikumbuke kosa letu milele. Tafazali, utuangalie, kwa maana sisi wote tuko watu wako. 10  Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa. Sayuni imekuwa jangwa,Yerusalemu imekuwa eneo lenye limeachwa.+ 11  Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*Kwenye mababu zetu walikusifu,Imeteketezwa kwa moto,+Na vitu vyote vyenye tulipenda sana vimeharibiwa. 12  Kwa sababu ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova? Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke sana?+

Maelezo ya Chini

Ao “kumungojea kwa uvumilivu.”
Ao “hezi.”
Tnn., “tuyeyuke.”
Tnn., “kwa mukono wa.”
Ao “Mwenye alitufanya.”
Ao “Hekalu letu la.”
Ao “uzuri.”