Isaya 64:1-12
64 Kama tu ungepasua mbingu na kushuka chini,Ili milima itetemeke kwa sababu yako,
2 Kama vile wakati moto unawasha miti midogo-midogo,Na moto unafanya maji yatokote,Basi jina lako lingejulikana kwa wapinzani wako,Na mataifa yangetetemeka mbele yako!
3 Wakati ulifanya mambo ya kuogopesha yenye hatukupima kutazamia,+Ulishuka, na milima ilitetemeka mbele yako.+
4 Tangu zamani hakuna mwenye alisikia wala kutega sikio,Wala hakuna jicho lenye lilimuona Mungu isipokuwa wewe,Mwenye kutenda kwa ajili ya wale wenye wanaendelea kumungojea.*+
5 Umekutana na wale wenye wanafurahia kutenda mambo yenye kuwa sawa,+Wale wenye wanakukumbuka na kufuata njia zako.
Angalia! Ulikuwa na kasirani kali, wakati huo sisi tuliendelea kutenda zambi,+Tulifanya vile kwa wakati murefu.
Je, sasa tuokolewe?
6 Na sisi wote tumekuwa kama mutu mwenye haiko safi,Na matendo yetu yote ya haki yako kama kipande cha nguo chenye mwanamuke anatumia katika siku zake za kuona mwezi.*+
Sisi wote tutakauka kama jani,Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.
7 Hakuna mwenye anaitia jina lako,Hakuna mwenye anajikaza kukushika,Kwa maana umetuficha uso wako,+Na unafanya tukuwe wazaifu* kwa sababu ya* kosa letu.
8 Lakini sasa, Ee Yehova, uko Baba yetu.+
Tuko udongo, na wewe uko Mufinyanzi wetu;*+Sisi wote tuko kazi ya mukono wako.
9 Usikasirike sana, Ee Yehova,+Na usikumbuke kosa letu milele.
Tafazali, utuangalie, kwa maana sisi wote tuko watu wako.
10 Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa.
Sayuni imekuwa jangwa,Yerusalemu imekuwa eneo lenye limeachwa.+
11 Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*Kwenye mababu zetu walikusifu,Imeteketezwa kwa moto,+Na vitu vyote vyenye tulipenda sana vimeharibiwa.
12 Kwa sababu ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova?
Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke sana?+
Maelezo ya Chini
^ Ao “kumungojea kwa uvumilivu.”
^ Ao “hezi.”
^ Tnn., “tuyeyuke.”
^ Tnn., “kwa mukono wa.”
^ Ao “Mwenye alitufanya.”
^ Ao “Hekalu letu la.”
^ Ao “uzuri.”