Isaya 22:1-25
22 Tangazo kuhusu Bonde la Maono:*+
Muko na shida gani yenye imewafanya ninyi wote mupande juu ya sehemu za juu za nyumba?
2 Ulijaa muvurugo,Muji wenye fujo, muji wenye furaha.
Watu wako wenye waliuawa hawakuuawa kwa upanga,Wala hawakukufa katika vita.+
3 Madikteta wako wote wamekimbia pamoja.+
Wamefanywa kuwa wafungwa bila kutumia upinde.
Wote wenye walipatikana walifanywa kuwa wafungwa.+
Hata kama walikuwa wamekimbilia mbali.
4 Ndiyo sababu nilisema: “Musiniangalie,Na mimi nitalia kwa uchungu.+
Musikazane kunifarijiKwa sababu ya kuharibiwa kwa binti ya* watu wangu.+
5 Kwa maana ni siku ya muvurugo na kushindwa na woga mukubwa,+Kutoka kwa Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi,Katika Bonde la Maono.
Ukuta unabomolewa,+Na kuko kilio kwenye mulima.
6 Elamu+ inabeba mufuko wa mishale,Pamoja na magari yenye watu na farasi,*Na Kiri+ inafunua* ngao.
7 Mabonde yako* ya muzuri zaidiYatajaa magari ya vita,Na farasi* watajipanga kwenye mulango mukubwa,
8 Na kitambaa cha kuficha cha Yuda kitaondolewa.*
“Siku hiyo utaangalia kuelekea depo ya silaha ya Nyumba ya Pori,+
9 na mutaona yale matundu mengi ya ukuta wa Muji wa Daudi.+ Na mutakusanya maji ya kiziwa cha maji cha chini.+
10 Mutahesabia nyumba za Yerusalemu, na mutabomoa nyumba ili kufanya ukuta ukuwe nguvu.
11 Na mutatengeneza beseni kati ya hizo kuta mbili kwa ajili ya maji ya kiziwa cha maji cha zamani, lakini hamutamuangalia Mutengenezaji wake Mukubwa, na hamutamuona Ule mwenye aliitengeneza zamani sana.
12 Siku hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi,Ataomba watu walie na kuomboleza,+Na kunyoa vichwa na kuvaa nguo za magunia.
13 Lakini kuliko kufanya vile, kuko kujifurahisha na kushangilia,Kuchinja ngombe na kuchinja kondoo,Kula nyama na kunywa divai.+
‘Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.’”+
14 Kisha Yehova wa majeshi akajifunua katika masikio yangu: “‘Kosa hili halitafunikwa kwa ajili yenu mupaka wakati mutakufa,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, anasema.”
15 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi, anasema: “Ingia kwa huyu musimamizi-nyumba, kwa Shebna,+ mwenye anasimamia nyumba,* na useme,
16 ‘Uko na nini hapa, na uko na nani hapa, ili ujichimbie kaburi hapa?’ Anachimba kaburi lake mahali pa juu; anajichongea mahali pa kupumuzikia* katika mwamba.
17 ‘Angalia! Yehova atakutupa chini kwa nguvu, Ee mwanaume, na kukushika kwa nguvu.
18 Hakika atakufunga sana na kukutupa kama mupira katika inchi pana. Utakufia kule, na kule magari yako yenye utukufu, yatakuwa haya kwa nyumba ya bwana wako.
19 Na nitakuondoa katika madaraka yako na kukufukuza katika cheo chako.
20 “‘Siku hiyo nitamuita mutumishi wangu Eliakimu+ mwana wa Hilkia,
21 na nitamuvalisha kanzu yako na nitamufunga muzuri kabisa kitambaa chako cha kujifunga kiuno kumuzunguka,+ na nitatia mamlaka yako katika mukono wake. Na atakuwa baba kwa wakaaji wa Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 Na nitatia funguo ya nyumba ya Daudi+ kwenye bega lake. Atafungua na hakuna mwenye atafunga; na atafunga na hakuna mwenye atafungua.
23 Nitamupigilia kama kipande kidogo cha muti mahali pa kudumu, na atakuwa kama kiti cha ufalme cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.
24 Na wataninginiza juu yake utukufu* wote wa nyumba ya baba yake, wazao na machipukizi,* vyombo vyote vidogo, vyombo vya umbo ya bakuli, na pia mitungi yote mikubwa.
25 “‘Siku hiyo,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema, ‘kile kipande kidogo cha muti chenye kimepigiliwa mahali pa kudumu kitaondolewa,+ na kitakatwa na kuanguka, na muzigo wenye kuwa juu yake utaanguka na kuharibiwa, kwa maana Yehova mwenyewe amesema.’”
Maelezo ya Chini
^ Inaonekana ni Yerusalemu.
^ Maneno ya kishairi yenye kutaja kitu kama mutu, pengine yanaonyesha sikitiko ao huruma.
^ Ao “wapanda-farasi.”
^ Ao “inatayarisha.”
^ Ao “Maeneo yako tambarare ya chini.”
^ Ao “wapanda-farasi.”
^ Ao “ulinzi wa Yuda utaondolewa.”
^ Ao “nyumba ya mufalme.”
^ Tnn., “makao.”
^ Tnn., “uzito.”
^ Ao “uzao.”