Isaya 59:1-21

  • Zambi za Israeli zinawatenga na Mungu (1-8)

  • Kuungama zambi (9-15a)

  • Yehova anaingilia kati kwa ajili ya wenye kutubu (15b-21)

59  Angalia! Mukono wa Yehova hauko mufupi sana usiweze kuokoa,+Wala sikio lake haliko nzito sana lisiweze kusikia.+   Hapana, makosa yenu wenyewe ndiyo yamewatenganisha na Mungu wenu.+ Zambi zenu zilimufanya awafiche uso wake,Na anakataa kuwasikia.+   Kwa maana mikono yenu imechafuliwa na damu+Na vidole vyenu vimechafuliwa na kosa. Midomo yenu inasema uongo,+ na ulimi wenu unasema ukosefu wa haki kwa sauti ya chini.   Hakuna mwenye anaita haki,+Na hakuna mwenye anaenda kwenye tribinali katika ukweli. Wanategemea jambo la kuwazia-wazia tu*+ na kusema mambo yenye hayana mafaa yoyote. Wanatunga mimba ya taabu na kuzaa jambo lenye kuumiza.+   Wanatotoa mayai ya nyoka mwenye sumu,Na wanasuka nyuzi za buibui.+ Kila mwenye anakula mayai yao atakufa,Na yai lenye kuvunjwa linatotoa nyoka-kipiri.   Nyuzi zao za buibui hazitatumika kama nguo,Wala hawatajifunika kile chenye wanatengeneza.+ Kazi zao ni zenye kuumiza,Na matendo ya jeuri yako katika mikono yao.+   Miguu yao inakimbilia kufanya uovu,Na wanafanya haraka ili kumwanga damu yenye haina kosa.+ Mawazo yao ni mawazo yenye kuumiza;Uharibifu na taabu viko katika njia zao.+   Hawakujua njia ya amani,Na hakuna haki katika njia zao.+ Wanapotosha barabara zao;Hakuna mwenye anatembea mule mwenye atapata amani.+   Ndiyo sababu haki iko mbali sana na sisi,Na uadilifu* hautufikie. Tunaendelea kutumainia mwangaza, lakini, angalia! kuko giza;Tunaendelea kutumainia uangavu, lakini tunaendelea kutembea katika weusi.+ 10  Tunapapasa tukitafuta ukuta kama vipofu;Tunaendelea kupapasa kama watu wenye hawana macho.+ Tunajikwaa katikati ya muchana kama katika giza la mangaribi;Kati ya wenye nguvu tuko kama vile wafu. 11  Sisi wote tunaendelea kunguruma kama dubuNa kulia kwa huzuni kama njiwa. Tunatumainia kupata haki, lakini hakuna;Tunatumainia kupata wokovu, lakini uko mbali sana na sisi. 12  Kwa maana maasi yetu ni mengi mbele yako;+Kila moja kati ya zambi zetu inashuhudia juu yetu.+ Kwa maana maasi yetu yako pamoja na sisi;Tunajua muzuri makosa yetu.+ 13  Tumemukosea na kumukana Yehova;Tumemugeuzia Mungu wetu migongo yetu. Tumesema kuhusu ukandamizaji na uasi;+Tumetunga uongo na kusema kwa sauti ya chini maneno ya uongo kutoka katika moyo.+ 14  Haki imerudishwa nyuma,+Na uadilifu* unasimama mbali;+Kwa maana kweli imejikwaa* katika kiwanja cha watu wote,Na jambo lenye kunyooka haliwezi kuingia. 15  Kweli imekosekana,*+Na kila mutu mwenye kuacha ubaya ananyanganywa. Yehova aliona jambo hilo na akachukizwa,*Kwa maana hapakukuwa haki.+ 16  Aliona kama hapakukuwa mutu,Na alishangaa kama hakuna mwenye aliingilia kati,Basi mukono wake ukaleta wokovu,*Na haki yake mwenyewe ikamutegemeza. 17  Kisha akavaa haki kama koti ya chuma,Na kofia ya chuma ya wokovu* juu ya kichwa chake.+ Alivaa nguo za kisasi kama nguo zake+Na kujifunga bidii kama koti.* 18  Atawapatia zawabu kulingana na matendo yao:+ Kasirani kali kwa wapinzani wake, malipo kwa maadui wake.+ Na atalipa visiwa kile chenye vinastahili. 19  Wataogopa jina la Yehova kuanzia mahali jua linashukiaNa utukufu wake kuanzia mahali jua linatokea,Kwa maana ataingia kama muto wenye kuenda haraka,Wenye kuendeshwa na roho ya Yehova. 20  “Mukombozi+ atakuja Sayuni,+Kwa wale wa Yakobo wenye wanaacha ukosaji,”+ ni vile Yehova anasema. 21  “Lakini mimi, hili ndilo agano langu pamoja nao,”+ ni vile Yehova anasema. “Roho yangu yenye kuwa juu yako na maneno yangu yenye nimetia katika kinywa chako—hayataondolewa katika kinywa chako, katika kinywa cha watoto wako,* ao katika kinywa cha wajukuu wako,”* ni vile Yehova anasema, “kuanzia sasa na milele.”

Maelezo ya Chini

Ao “jambo la bure-bure.”
Ao “unyoofu umejikwaa.”
Ao “Unyoofu umekosekana.”
Tnn., “na jambo hilo lilikuwa la mubaya katika macho yake.”
Ao “ukamuletea ushindi.”
Ao “ushindi.”
Ao “koti yenye haina mikono.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “katika mbegu ya mbegu yako.”